
Bunge la Uganda likiendelea na kikao. Picha imetumiwa kwa ruhusa ya Taasisi ya Parliament Watch Uganda.
Wananchi wa Uganda wanatumia vizuri mitandao ya kijamii kuwasiliana na wabunge wao, kwa msaada wa Parliament Watch Uganda, taasisi inayofuatilia shughuli za Bunge la Uganda na kisha kutoa takwimu zinazohitajika pamoja na uchambuzi wa kitaalam.
Mnamo Februari 26, 2015, taasisi hiyo iliandaa Mjadala ulioitwa #MPsEngage na kufanyika kwenye mtandao wa Twita ili kuwapa fursa wabunge wanawake kuzungumzia mada iliyoitwa, “Kuwafanya Wanawake Wathaminike kwenye Mchakato wa Kibunge’. Wahudhuriaji walikuwa wa aina tatu na kwa wakati ule ule: Watu wa Gulu kaskazini mwa Uganda, wabunge wanawake wa Uganda na watumiaji wa mitandao ya kijamii nchini Uganda.
Gulu ni wilaya iliyokuwa na misuguano Kaskazini mwa Uganda. Kilikuwa ni kitovu cha mgogoro kati ya serikali ya Uganda na waasi wa Lord’s Resistance Army (LRA). Wanawake wa eneo hilo wanakabiliwa na changamoto nyingi ambazo ni athari za vita na kupuuzwa na serikali kuu.
Wahudhuriaji kutoka Gulu waliuliza maswali kupitia vinasa sauti, na wataalamu wa mitandao ya kijamii walitwiti maswali hayo kwa wabunge.
Wakati wa majadiliano hayo, wabunge wanawake walitakiwa kuelezea mafanikio na changamoto walizokabiliana nazo wakati wote wa kipindi cha uongozi wao.
Watumiaji wa mitandao ya kijamii walitoa maoni, kunukuu na kuwaelekeza wafuatiaji wao kwenye alama ishara ya majadiiano hayo ambayo ilikuwa ni #MPsEngage.
Do women in Uganda have full access to participation in all political process and decision making in UG? #MPsEngage pic.twitter.com/8Oz5PlWDk1
— Parliament Watch (@pwatchug) February 25, 2015
Je, wanawake nchini Uganda wanapata ushiriki katika katika michakato yote ya kisiasa na kufanya maamuzi nchini Uganda?
Mwandishi wa Uganda, ambaye pia ni mwanablogu Raymond Qatahar alikuwa na haya ya kuchangia:
Taking an observatory eye into the #MPsEngage . Glad that finally, a technological solution has been found to connect legislators to p'ple
— Qatahar Raymond (@qataharraymond) February 26, 2015
Ninafuatilia majadiliano ya #MPsEngage. Nina furaha kwamba hatimaye, suluhisho ya kiteknolojia limepatikana na kuwaunganisha wabunge na wananchi
Jackie Asiimwe, Mwanasheria ya Uganda, aliuliza:
When will we ever ask male MPs how they are advancing the cause of women, because they too are voted by and represent women. #MPsEngage
— Jacqueline Asiimwe (@asiimwe4justice) February 26, 2015
Ni lini tutapata fursa ya kuwauliza wabunge wanaume namna wanavyoshughulikia masuala ya wanawake, kwa sababu na wao pia walichaguliwa na wanawawakilisha wanawake
Kollin Rukundo aliibua suala la muswada wa ndoa na talaka . Muswada huo, pamoja na mambo mengine, unawalazimisha wanandoa kuwa na umiliki sawa wa mali zao, na kuwafanya wenzi wanaoishi pamoja bila ndoa kuwa na haki za kumiliki mali na pia unafanya ubakaji unaofanyika kati ya wanandoa kuwa kosa la jinai:
Referring to Marriage & Divorce Bill “How can an MP pick one clause(divorce) and use it demonise the entire bill?”- Miria Matembe #MPsEngage
— Kollin Rukundo T (@kollinsayz) February 26, 2015
Kwa kurejea muswada wa Ndoa na Talaka, “Namna gani Mbunge anaweza kuchukua kipengele kimoja (talaka) na kukitumia kupinga muswada mzima?
Akimnukuu Miria Matembe, waziri wa zamani wa maadili na uadilifu, Jackie Asiimwe alisema:
MPs don't use their power properly. Instead they do the work of the Executive – building schools, supplying medicines – Matembe #MPsEngage
— Jacqueline Asiimwe (@asiimwe4justice) February 26, 2015
Wabunge hawatumii mamlaka yao ipasavyo. Badala yake wanafanya kazi za Serikali -kujenga shule, kununua madawa – Matembe
Daniel Turitwenka, mshauri mwelekezi wa mitandao ya kijamii, aliweka picha ya mshiriki wa Gulu, kaskazini mwa Uganda, akishiriki moja kwa moja kwa njia ya simu wakati wa mjadala huo:
#Gulu had a live phone conversation with @UWOPA chair Betty Amongi – answering and directly #MPsEngage pic.twitter.com/R5IvjNyy46
— Danny T (@DannyT_UG) February 26, 2015
Wakazi wa Gulu walikuwa na majadiliano ya moja kwa moja kwa njia ya simu na Mwenyekiti wa Asasi ya UWOPA, Betty Among – maswali yalijibiwa na moja kwa moja
Alimnukuu mmoja wa washiriki:
#Gulu Mr Okello says separation of children and parents is an issue and urges @pwatchug to keep bringing the MPs to answer qns #MPsEngage
— Danny T (@DannyT_UG) February 26, 2015
Bw Okello anasema kutengana kwa watoto na wazazi ni suala gumu na aliwasihi @pwatchug kuendelea kuwaleta wabunge wajibu maswali
Wakazi wa Gulu walijitahidi kufanya mahitaji yao yafahamike:
#Gulu everyone should have access to reproductive health. still a lot of women lack this! #MPsEngage pic.twitter.com/DzYSvJNHyj
— Parliament Watch (@pwatchug) February 26, 2015
Hapa Gulu kila mmoja lazima apate huduma za afya ya uzazi. Bado wanawake wengi hawana huduma hizi
Suala la huduma duni za ukunga lililalamikiwa:
#Gulu “our women die every day and night because of lack of midwives! This can not be tolerated!” #MPsEngage pic.twitter.com/yVat6StZEg
— Danny T (@DannyT_UG) February 26, 2015
Wanawake wetu wengi wanapoteza maisha mchana na usiku kwa sababu ya kukosekana kwa wakunga! Hali hii haivumiliki!
Ingawa mazungumzo hayo yalifanyika kwenye mtandao wa Twita, Denis R Tumusiime alibaini kwamba wabunge wanawake bado hawajaweza kutumia vizuri mitandao ya kijamii kufanya shughuli zao:
@deejahn @she_infinite I am yet to see a tweet from a female mp. #MPsEngage
— Dennis R. Tusiime (@drwatooro) February 26, 2015
Bado sijaona twiti kutoka kwa mbunge mwanamke
Wakati mjadala huo ukielekea ukingoni, Jackie Asiimwe, ambaye ni mwanasheria, alishauri kwamba ushiriki huo usiishie hapo:
Our time here is coming to an end, but the conversation continues. We must all engage our MPs all the time. #MPsEngage
— Jacqueline Asiimwe (@asiimwe4justice) February 26, 2015
Muda wetu unakaribia kuisha, lakini mazungumzo yaendelee. Lazima tuwasiliane na wabunge wetu muda wote