
Mkimbiaji wa Mashindano ya Paralimpiki Oscar Pistorius akiwa kizimbani. Mei 5, 2014 Imepigwa na Ihsaan Haffejee. Haki Miliki ya Demotix.
Oscar Pistorius, mkimbiaji mwenye ulemavu wa miguu wa Afrika ya Kusini alipatwa na hatia ya mauaji ya bila kukusudia kwa kumpiga risasi rafiki yake wa kike mwaka jana, amehukumiwa kifungo cha mpaka miaka mitano gerezani. Kadhalika atatumikia miaka mingine mitatu nje ya gereza kwa kosa la matumizi ya silaha kinyume cha sheria.
Pistorius anasema alidhani Reeva Steenkamp alikuwa ni kibaka aliyekuwa kaingia kwake kwa kuvunja nyumba kupitia dirisha la bafuni. Serikali, kwa mujibu wa Jaji Thokozile Masipa, ilishindwa kuthibitisha pasipo mashaka yoyote kwamba Pistorius alikusudia kumwua.
Shauri hilo, ambalo ni tukio kubwa la mitandao ya kijamii nchini Afrika Kusini, lililoibua hisia kubwa pamoja na ufuatiliaji mkubwa wa vyombo vya habari. Kifungo chake kimelinganisha na kifungo cha miaka 77 alichohukumiwa jangili wa faru mwezi Julai, kilichowashangaza na kuwatia hasira watumiaji wengi wa mitandao ya Twita.
Wengine wanadhani jaji alikuwa mpole sana, ushahidi wa kuharibika kwa mfumo wa haki nchini Afrika Kusini:
Utterly pathetic verdict. Makes a mockery of human life to be sentenced to less for killing than for fraud. Disgusting. #OscarPistorius
— David Talbot (@davidtalbot59) October 21, 2014
Hukumu ya kijinga sana. Inakejeli uhai wa mwanadamu kutoa hukumu ndogo kwa mauaji kuzidi ufisadi. Inakera
#oscarpistorius 5 years? He could be out in 2 years –NOT GOOD ENOUGH!!!
— Dame Jana Hitchens-M (@offlinesometime) October 21, 2014
Miaka mitano? Na anaweza kutoka ndani ya miaka miwili –HAIJAKAA POA
Chini ya sheria ya Afrika Kusini, anaweza kuwa huru baada ya miezi nane tu.
Stefanie Ship aliuliza:
What is wrong with this world in that you kill someone & only get 5 years imprisonment?! Is somebody only worth 5 years?! #OscarPistorius
— Stefanie Ship (@stefanieshipman) October 21, 2014
Nini kimeharibika kwenye dunia hii ambapo unamwua mtu na kuishia kuhukumiwa miaka mitano jela? Maisha ya mtu yana thamani ya miaka mitano?!
Remember – 5 year sentence means he could be free after not much more than 2 years. #OscarPistorius
— andrew harding (@BBCAndrewH) October 21, 2014
Kumbuka hukumu ya miaka mitano ina maana anaweza kutoka jela si zaidi ya miaka miwili
#OscarPistorius today women find out that our life is worth less than a logo on a training shoe perhaps!
— Louise (@louisebro66) October 21, 2014
Leo hii wanawake tunajikuta maisha yetu labda hayana thamani zaidi ya nembo zinazotumika kwenye viatu vya mazoezi
you are a disgrace #Masipa NO JUSTICE 4Steenkamps & a travesty to womens’ rights /domestic abuse (which you deny in yr sentence)#OscarTrial
— Ms Marwood Black (@Marwood20) October 21, 2014
Masipa unajitafutia laana bure. Hukutenda haki kwa kifo cha Steenkamps. Ni pigo kwa haki za wanawake na si haki kabisa kwa vitendo vya udhalilishaji wa majumbani (umekataa kutambua matatizo hayo kwenye hukumu yako)
I know it was not about satisfying the society, but I would have liked the years to be 10 at least! #OscarPistorius #OscarTrial
— Sibusiso Mgidi (@SibusisoMgidi1) October 21, 2014
Ninajua haikuwa kwa lengo la kuridhisha jamii, lakini ningependa angalau hukumu imefikia miaka kumi!
The trial was longer than how long Oscar will spend in jail. #OscarTrial
— Prince Akeem (@tackyz) October 21, 2014
Shauri hilo haikuchukua muda mrefu kuzidi muda ambao Oscar atausotea jela
Kwenye mtandao wa Facebook, Thapelo Tips Seemise alifananisha hukumu hiyo na muda uliopita tangu mauaji ya Steenkamp yafanyike:
Ilichukua miaka miwili kufikia hitimisho la hukumu ya miaka mitano jela!!! Haki ni suala lisilowezekana nchini mwangu
Wengine, hata hivyo, waliunga mkono hukumu hiyo:
@ChrisWragge Agreed. Still, 5 yrs is better than community service, which is where the Judge seemed headed. #OscarPistorius @CBSNewYork
— KK Smith (@sassy_kk) October 21, 2014
Ninaunga mkono. Bado, hata hivyo miaka mitano ni nafadhali itumike kwa kuihudumia jamii, jambo ambalo nadhani ndilo Jaji alilomaanisha
So many people to quick to judge Oscar as if they're perfect, he got prison time so be happy and stop complaining. #OscarTrial
— Nqobile (@Iam_nqobs) October 21, 2014
Watu wnegi wana haraka ya kumhukumu Oscar utafikiri wao hawajawahi kukosea. Haya basi amehukumiwa chekeleeni na mwache kulalamika
Regardless of what we think Judge Masipa really understands the purpose of #Judgment, its for #Reconciliation not #Condemnation #OscarTrial
— Prosper Ntuli (@Proetic) October 21, 2014
Bila kujali vile tunavyofikiria Jaji Masipa alielewa kwa hakika lengo la hukumu. Ni kupatanisha watu sio kutafuta mkosaji
Not everyone will agree w/ sentence. Light. But #JudgeMasipa had well reasoned argument reaching sentence. #OscarSentence #OscarTrial.
— Thebe Ikalafeng (@ThebeIkalafeng) October 21, 2014
Si kila mtu anaweza kukubaliana na hukumu hiyo. Lakini Jaji Masipa alikuwa na hoja inayoeleweka kutoa hukumu
People mustn't make conclusions here and insult and act pathetic towards our Law. There's appeal that looks more possible.#OscarTrial
— MTHOKO HLELA•✌️ (@MahatmaDUTCH_7) October 21, 2014
Watu muache kufanya mahitimisho hapa na kuilaani na kukejeli sheria yetu. Vinginevyo kuna uwezekano wa rufaa
Wengine walifanya hukumu hiyo iwe kichekesho:
I expect a book trilogy release ‘How To Get Away With Murder’ #OscarPistorius
— Jess Espin (@JessEspinX) October 21, 2014
Natarajia kuagiza toleo jipya la kitabu kinachoitwa, “Nani ya kukwepa mkono wa sheria unapoua’
So…. who's buying the movie rights? I personally think Universal is overdone. #Oscartrial
— Felicia Mosiane (@FeliciaT_Mos) October 21, 2014
Sasa…nani ananunua haki miliki ya sinema hiyo? Binafsi nadhani alama ya INAFAA KWA YEYOTE imepitiliza
@EFF_Supporters Lol that's why Dewani came here to kill his wife bruh. #OscarTrial
— Charmagne Ledwaba (@LedWhat) October 21, 2014
Du. Kumbe ndio maana Dewani amekuja na hapa kumwuua mke wake
Shrien Dewani ni Mwingereza anayetuhumiwa kula njama kupanga mipango ya kuwezesha mke wake Anni Dewani auawe wakati wakiwa kwenye fungate nchini Afrika Kusini. Shauri lake linaendelea nchini Afrika Kusini.