- Global Voices in Swahili - https://sw.globalvoices.org -

Uchafu Kutoka Viwandani Waua Mamia ya Ndege wa Porini Nchini Mongolia

Mada za Habari: Asia Mashariki, China, Mazingira, Uandishi wa Habari za Kiraia

Zaidi ya ndege wa majini 500 wameonekana wakiwa wamekufa katika eneo la maziwa nchini Mongolia tangu kuanza kwa majira ya kipindi cha joto kutokana na maji kuchafuliwa. Maji hayo machafu, kama ilivyotaarifiwa na wafugaji wa maeneo hayo, maji haya yaliyochanganyikana na taka sumu yalitoka katika eneo la viwanda. Annie Lee kutoka tovuti ya China Hush aliandika [1] habari picha ya hali halisi ya tukio hili.