- Global Voices in Swahili - https://sw.globalvoices.org -

Serikali ya Marekani Yadai Takwimu za Shirika la Indymedia Athens

Mada za Habari: Marekani ya Kaskazini, Marekani, Uandishi wa Habari za Kiraia
Imagen en Flickr del usuario Tim Pierce (CC BY 2.0).

Picha kwenye mtandao wa Flickr na Tim Pierce [1] (CC BY 2.0).

Mnamo Septemba 5, Wizara ya Sheria ya Marekani iliitaka shirika linaloshughulika na masuala ya kuhifadhi tovuti iitwayo  May First [2] kutoa taarifa za mmoja wa wateja wake, ambaye ni Kituo cha Ugiriki cha cha Uandishi Huru Athens, kinachofahamika kama Indymedia Athens [3]. Likiwa limeanzishwa mwaka 2005, May First ni shirika lisilo la kibiashara linalojikita katika kutoa huduma za mtandao wa Intaneti, kama vile kuhifadhi tovuti za watu binafsi na mashirika. Taarifa zinazotakiwa na Idara ya Usalama ni habari maalum kutoka kwenye akaunti ya Indymedia Athens, iliyohifadhiwa kwenye vihifadhi takwimu (servers) za May First.

Katika  tamko [4], May First ilibainisha kwamba dai hilo linaweza kutafsiriwa kama jaribio la serikali ya Marekani kuisaidia serikali ya Ugiriki. Kadhalika, walibainisha kwamba hawatatoa taarifa zinazotakiwa labda ikiwa Kituo cha Uhuru wa Habari Athens kitazihitaji –wanasema kwamba kukubaliana na agizo hilo ni kuingilia haki ya faragha.

Kwa sasa, wanasheria wa Electronic Frontier Foundation, ambao wanaiwakilisha May First, wanawasiliana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Marekani. Wakati wa kuchapishwa kwa habari hii, maafisa wa serikali wa Marekani hawajatoa maelezo yoyote kuhusu malengo hasa ya takwimu zinazodaiwa.