Wa-Palestina wanasema mvua ya moto inanyesha Gaza, baada ya Israeli kuanza operesheni ya ardhini [1] ndani ya eneo inalolizunguka, Gaza. Gaza, inayoelezwa kama gereza la wazi, ndiko wanakoishi wa-Palestina milioni 2, ambao hawana pa kukimbilia. Israeli inapakana na Gaza upande mmoj, na Misri inaifungia kwenye upande mwingine.
Kwenye mtandao wa Twita, Jehan Alfarra, mwenye wafuasi 8,000 anasema:
NOW: It's raining FIRE on #Gaza [2] tonight with an Israeli ground invasion on the wayyy! #PrayForGaza [3] pic.twitter.com/QMOTBduZ96 [4]
— Jehan Alfarra (@palinoia) July 17, 2014 [5]
Gaza usiku huu inakabiliana na uvaizi wa ardhini unaofanywa na Israeli!
Mtumiaji mwingine aitwaye Gaza Writes Back, mwenye wafuasi 36,400 kwenye mtandao wa Twita, anasema kuanza kwa uvamizi wa ardhini na milipuko mizito ya mabomu imeifanya “Gaza yote kuwa mithili ya mpira wa moto”:
israel starts a land invasion and turns the whole Gaza Strip into a ball of fire… #GazaUnderAttack [6] pic.twitter.com/pnyFbdtcra [7] — Gaza Writes Back (@ThisIsGaZa) July 17, 2014 [8]
Israeli imeanza uvamizi wa ardhini na kuugeuza ukanda wote wa Gaza kuwa mithili ya mpira wa moto
Na iFalasteen, vile vile akitokea Gaza, alitwiti kwa wafuasi wake 26,800:
It's raining bombs across Gaza Strip now from sea, land and air… Israel is bombing everything… #GazaUnderAttack [6]
— فلسطين i (@iFalasteen) July 17, 2014 [9]
Mvua ya mabomu inanyesha kwenye ukanda wa Gaza sasa hivi kutoka baharini, ardhini na hewani…Israeli inapiga mabomu pande zote
Pia mtumiaji mwingine akiwa Gaza, Palestine, anatuma picha hii ya milipuko ya mabomu ukanda wa Gaza usiku huu kwa wafuasi wake 10,000 kwenye mtandao wa Twita:
it's the heaviest attack now !! #PrayForGaza [3] #GazaUnderAttack [6] pic.twitter.com/VNWN6Dlaui [10] — Palestine | פלסטינה (@iPalestinian91) July 17, 2014 [11]
Ni shambulio zito linaendelea sasa!!
Kwenye picha nyingine, anasema:
Even the moon is red in Gaza tonight… #GazaUnderAttack [6] pic.twitter.com/EtgQgkyyTX [12]
— فلسطين i (@iFalasteen) July 17, 2014 [13]
Hata mwezi umekuwa mwekundu hapa Gaza usiku wa leo
Mpiga picha Jehad Saftawi anatuma picha kutoka kwenye mpaka wa Gaza, ikionyesha kuanza kwa operesheni hiyo:
The Israeli ground invasion has started on Gaza Strip, here the borders of Gaza. #GazaUnderAttack [6] pic.twitter.com/ny7sEjhar0 [14]
— Jehad Saftawi (@Jehadsaftawi) July 17, 2014 [15]
Shambulio la ardhini linalofanywa na Israeli limeanza kwenye ukanda wa Gaza, hapa kwenye mpaka wa Gaza
Wakati Lara Abu Ramadan, mwandishi wa habari wa ki-Palestina, mfasiri na mpiga picha wa kujitegemea anayeishi Gaza, anaeleza:
This is horrible I can see a huge fire from the Israeli tanks western Gaza strip. #GazaUnderAttack [6] pic.twitter.com/whpSbRmSpo [16]
— Lara (@laraaburamadan) July 17, 2014 [17]
Hali inatisha. Naweza kuona moto mkubwa kutoka kwenye matanki ya Israeli magharibi mwa ukanda wa Gaza
Na mwanablogu wa ki-Palestina Haitham Sabbah, anatoa kiungo hiki cha habari a moja kwa moja kutoka Gaza:
Online Live Stream From #GazaUnderAttack [6] http://t.co/jg2PZQbXXK [18] — Haitham Sabbah (@sabbah) July 17, 2014 [19]
Habari za moja kwa moja kuhusu shambulio linaloendelea Gaza #GazaUnderAttack [6] http://t.co/jg2PZQbXXK [18] — Haitham Sabbah (@sabbah)
Wakati huo huo, mwandishi wa habari Richard Hall, anayeishi Paris, anawakumbusha wafuasi wake 6,000:
Last time Israel invaded Gaza 1,387 Palestinians were killed. 773 were civilians, including 320 children and 109 women. (Source: B'Tselem)
— Richard Hall (@_RichardHall) July 17, 2014 [20]
Mara ya mwisho Israeli kuivamia Gaza, wa-Palestina 1,387 waliuawa. 773 walikuwa wananchi wasio wanajeshi, wakiwemo watoto 320 na wanawake 109 (Chanzo: B'Tselem)
Leo ni siku ya 11 tangu kuanza kwa “Operesheni ya Kujilinda”, ambayo imepoteza maisha ya wa-Palestina 230, wakiwemo wanawake na watoto, na zaidi ya watu 1,500 wakijeruhiwa.
Kutoka Gaza, Hamas, ambayo imeutawala ukanda huo tangu mwaka 2007, ililipua makombora [21] kwenda Israeli. Roketi nyingi zinazoingia Israeli hazijasababisha madhara makubwa, kwa sababu, kwa kiasi fulani, ya mfumo wa anga wa ulinzi unaofadhiliwa na Marekani, ambao umezuia makombora yapatayo 70 mpaka sasa, [22] kwa mujibu wa gazeti la the Guardian.
Kwa operesheni hii ya kimakundi, madhara yanaweza kuongezeka zaidi.