Madege ya Kijeshi ya ki-Palestina Yaruka kwenye Anga la Israel

Brigedi ya Palestina ya Al Qassam, tawi la kijeshi la Hamas, lilionyesha miundo mitatu ya madege ya kijeshi leo, ikisema kuwa yalirushwa kwenye anga la Israel.

Mwandishi Dima Khatib anatwiti:

Brigedi ya Al Qassam inasema walitengeneza aina tatu za madege ya kijeshi ya Ababil: A1A, A1B, A1C picha @QudsN ya A1B wakati wa zoezi hilo la kijeshi

Madege hayo, yaliyotengenezwa Palestina, yanaitwa Ababil – jina la ndege waliotajwa kwenye Quran tukufu, walioilinda Mecca wakati wa vita na Yemen mwaka 571.

Mwanablogu wa Gaza Jehan Alfarra aliandika:

Nimeshangazwa na matumizi ya madege ya kijeshi yanayofanywa na Mamlaka ya Palestina kwenye ukanda wa Gaza. Tuko kwenye hatari

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.