Yametimu majuma mawili tangu ghasia dhidi ya Waislamu [1] kwenye majiji ya pwani nchini Sri Lank- Aluthgama na Beruwala. Ingawa hali imetulia baada ya kulaaniwa sana [2] kila sehemu, bado ghasia hizo dhidi ya Waislamu zinaendelea [3] katika maeneo tofauti ya Sri Lanka.
Mwanablogu Abdul Khaleq [4] anatwiti kuhusu tukio moja huko Ratmalana [5] sehemu ya wilaya ya Colombo:
Ratmalana Borupona Rd mosque set on fire 1am. Flames spotted early and put out. Min Fowzie here #StayStrongSrilanka [6] pic.twitter.com/Vys16T51vn [7]
— abdulkhaleq (@HalikAzeez) June 29, 2014 [4]
Msikiti ulioko barabara ya Ratmalana Borupona umechomwa moto saa 7 usiku. Moto ulioanza mapema ulizimwa.
Mwanablogu D. B. S. Jeyaraj [8] ana habari zaidi kuhusu jaribio lililoshindwa la kushambulia msikiti wa Thalayan Bawa Jumma uliopo kwenye barabara ya Borupane mjini Ratmalana masaa ya asubuhi Jumapili iliyopita, tarehe 29 Juni, 2014.