Mapigano ya Wanakijiji Kugombea Ardhi Yasababisha Maafa Nchini Madagaska

Blogu ya L'Express Mada ilitoa taarifa kwamba kijiji kizima cha Andranondambo kilichoko Kusini mwa Madagascar kiliharibiwa [fr] kufuatia mapigano ya wanakijiji yaliyosababishwa na mzozo wa kumiliki ardhi. Vita vya wenyewe kwa wenyewe, ambayo ilidumu kwa siku tatu kati ya Mei 20-22, ilipoteza maisha ya wanakijiji wote. Akikumbuka tukio hilo, mmoja wa maafisa wa polisi anasimulia [fr]:

A notre arrivée, un chien errant était en train de dévorer un bras arraché d’ un corps. Dans une maison anéantie par les flammes, nous avons mis la main sur une dépouille. L’air était irrespirable [..] Même l’école publique et l’église d’Andranondambo ont été ravagées. Les toitures en tôle ont été arrachées avec tous les mobiliers.

Tulipowasili, mbwa alikuwa akila mabaki ya maiti. Katika nyumba jirani iliyokuwa imeharibiwa kwa moto, tulikuta maiti zaidi na uvundo usiovumilika. Hata shule za umma na makanisa vyote vilikuwa zimeharibiwa. Vifaa vyote kutoka kwa nyumba vilikuwa vimetawanyika.

Mgogoro wa ardhi ulianza mwaka wa 1991 wakati madini ya mica yilipogunduliwa katika kijiji hicho cha Andranondambo. Kukimbilia kwa wachimbaji wa ardhi kulipelekea wanakijiji kuhamia mbali katika kijiji kingine cha Ambatotsivala. Tangu wakati huo, vijiji hivi viwili vimekuwa na mgogoro juu ya haki za ardhi lakini mgogoro haujawahi kufikia kiwango cha taabu ya vurugu hadi hivi karibuni.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.