Hong Kong: Mfanyakazi wa Ndani Apigwa Makofi, Mateke na Kulazimishwa Kufanya Kazi Masaa 21 kwa Siku
· Imeandikwa na Oiwan Lam Imetafsiriwa na Joyce Maina
Mada za Habari: Asia Mashariki, Hong Kong (China), Habari za Wafanyakazi, Haki za Binadamu, Uandishi wa Habari za KiraiaKesi nyingine ya unyanyasaji wa mtumishi wa ndani wa kigeni imefichuliwa. Mhanga huyo Rowena Uychiat inadaiwa alilazimishwa kufanya kazi masaa 21 kwa siku (6:00 mpaka 03:00) bila kupewa siku ya mapumziko. Alidai kupigwa makofi, mateke, kutukanwa kwa maneno vibaya na nywele zake kuvutwa. Tom Grundy aliripoti [1] tukio hilo kwa undani.