Watu wasiopungua watatu walikufa na kati ya watu 25 na 30 wamenaswa baada ya kuanguka kwa mgodi ulikuwa unaendeshwa kinyume cha sheria katika idara ya Cauca [1], kusini magharibi mwa Colombia, kama ilivyoripotiwa [2] [es] na vyombo vya habari mnamo Alhamisi, Mei 1.
HSBNoticias aliarifu kwenye mtandao wa Twita:
[FOTOS] [+18] Se lleva a cabo el rescate de 25 a 30 mineros atrapados en una mina del #Cauca [3] ➜http://t.co/Cm0XpWdYFq [4] pic.twitter.com/6xpfKFDLS4 [5]
— HSBNOTICIAS (@HSBNOTICIAS) Mayo 1, 2014 [6]
[PICHA] juhudi za uokoaji kuwatafuta wachimbaji 25 hadi 30 walionaswa katika mgodi katika idara ya Cauca.