Chui [2] wameorodheshwa kama wanyama wanaoishi kwenye mazingira magumu [3] [zh] nchini Taiwan. Kwa kuwa chui wakubwa huishi misituni na mwituni katika maeneo tambarare na yale yenye milima na makazi yao ni aina tofauti sana [4]. Makazi yao nchini Taiwan yanasumbuliwa kwa sababu ya miradi mipya ya ujenzi. Kamati ya tathmini ya mazingira ya Taiwan ilikuwa imekataa kwa muda ombi kutoka Serikali ya Miaoli kuendeleza barabara mbadala katika Miaoli inayopita katikati ya makazi ya chui mnamo Aprili 16 2014 baada ya kusambaa maandamano [5] na malalamiko ya kusitishwa mradi huo [6]. Hata hivyo, mradi huu wa maendeleo haukusimamishwa, na miradi ya maendeleo zaidi katika eneo hili inaendelea kubuniwa. Ukurasa wa facebook [1] [zh] ulianzishwa ili watu ambao wanaotaka kuwalinda chui nchini Taiwan waweza kupata taarifa vizuri na kuhamasishwa.
Wito wa Kuacha Ujenzi Nchini Taiwan Ili Kuwalinda Chui
· Imeandikwa na I-fan Lin Imetafsiriwa na Joyce Maina
Mada za Habari: Asia Mashariki, Taiwan (ROC), Maandamano, Maendeleo, Mazingira, Uandishi wa Habari za Kiraia