Watu 28 Wafariki, 268 Bado Hawajulikani Walipo Baada ya Feri ya Korea Kusini Kuzama

Feri ya Korea Kusini iliyokuwa inaelekea kwenye kisiwa cha mapumziko ilizama mnamo Aprili 16, 2014 na mamia ya abiria, ikiwa ni pamoja na wanafunzi 325 wa shule ya sekondari waliokuwemo. Zimetimia siku mbili tangu ajali hiyo itokee na watu 28 wamethibitika kufariki kufikia Aprili 18 na watu 268 bado hawajulikani walipo. Uwezekano wa kupona ni mdogo mno.

Picha tatu hapa chini zimetolewa hadharani kupitia ukurasa wa Facebook wa Coast Guard [ko]. Picha ya kwanza inaonyesha nahodha wa mashua akiwa miongoni mwa kundi la kwanza kuokolewa.

Image of the rescue operation, Image shared by Korean Coast Guard

Picha imetolewa kwa umma na Ukurasa wa Facebook wa Coast Guard wa Korea Kusini

Image of Sewol ferry rescue operation, Image shared by Korean Coast Guard

Picha ya Feri ya Sewol katika operesheni ya uokoaji, picha kwa hisani ya Ukurasa wa Facebook wa Coast Guard wa Korea Kusini

Image of Rescue Operation, Image shared by Korean Coast Guard's Facebook page

Picha ya operesheni ya uokoaji, kwa hisani ya Ukurasa wa Facebook wa Coast Guard wa Korea Kusini

Mijadala ya mtandaoni nchini Korea Kusini imefurika salamu za rambirambi kwa waathirika na wapendwa wao pamoja na hasira kali dhidi ya nahodha na wafanyakazi ambao waliokolewa mapema zaidi kabla ya abiria. Kilichochochea hasira zaidi ni tangazo linalosemekana kutolewa kwenye feri hiyo kuwaambia abiria waendelee kubaki ndani [ko], hata wakati feri ilipoanza kuzama.

Mwaka 2003 wakati wa maafa ya moto ya reli ya chini ya ardhi ya Daegu, idadi kubwa ya abiria walikufa wakati kondakta wa treni alikimbia baada ya kukwanyua ufunguo. Mimi nasikia masimulizi kuwa nahodha wa feri ya Sewol na kondakta waliokolewa mapema. Ningependa iwe ni uongo mtupu. Kama hiyo ni kweli, basi hawawezi kusamehewa wala kuepuka adhabu.

Nahodha, baada ya kuagiza mfanyakazi wa kike wa ngazi ya chini kutangaza kwamba abiria wanatakiwa kukaa mahali walipo, alitoroka vizuri kabla ya mtu mwingine yeyote. Inanikumbusha tukio la kihistoria wakati wa Vita vya Korea – wakati Rais Rhee Seung-man, baada ya kutangaza kwamba “sasa hali ni shwari”, walikimbia baada ya kukata daraja mto Han. Imekuwa ni zaidi ya miaka 60, lakini historia inajirudia.

Mamlaka bado haijaweza kuthibitisha nini kilichosababisha tukio hilo, na uvumi mbalimbali imeibuka, ikiwa ni pamoja na feri inaweza kuwa iligonga mwamba. Hivi sasa, wengi wanatoa lawama kwamba meli ilifanyiwa utengenezaji kinyume cha sheria[ko] ili kuwabeba abiria zaidi. Watumiaji mtandao Korea wakijadili siri ambazo hazijatatuliwa.

Kuna maswali yaliyobaki: 1) jinsi gani feri ilizama katika eneo hilo na hakuna mwamba na hali ya hewa ilikuwa nzuri siku hiyo 2) Upande wa kulia wa sehemu kuu ya Feri kumebonyea sana. 3) Tangazo la “kaeni mlipo” wakati meli ilianza kuzama4) wafanyakazi na nahodha kuokolewa kwanza 5) wito wa dhiki ulifanywa saa 8:58 na abiria 6) mvuvi mdogo kuona kuna kitu kisicho sawa na Sewol saa 7:30.

Wengi walilaumu hisia na kuchukulia urahisi kupitia kwa vyombo vya habari.

Kama ukiangalia ripoti ya awali ya gazeti la Munhwa, unaweza kuona jinsi walikuwa wavivu katika kuripoti suala hili. Mazungumzo MBC kuhusu fedha za [bima] hata kabla ya operesheni ya kuwaokoa kumalizika. KBS inalenga zaidi juu ya majibu ya rais kuliko waathirika na taarifa juu ya ujumbe wa kuwaokoa (kupitia mwanabloglu kwenye mtandao kupitia alama ashiria “Mimi ni Peter”)

Ujumbe wa kuwaokoa unaendelea. Hata hivyo, jamaa na familia ya waathirika walitoa taarifa [ko] kukemea kwamba bado hakuna taarifa zinazoeleweka pamoja na habari za kutiwa chumvi kuhusu ukubwa wa timu ya waokoaji.

도착시간 5시 30분쯤 진도 실내체육관 비상상황실에 와보니 책임을 가지고 상황을 정확히 판단해주는 관계자가 아무도 없었습니다다. 심지어 상황실도 없었습니다다.[…] 어제 현장을 방문했습니다. 인원은 200명도 안됐고, 헬기는 단 두대. 배는 군함 두척. 경비정 2척. 특수부대 보트 6대. 민간구조대원 8명이 구조작업 했습니다다. 9시 대한민국 재난본부에서는 인원 투입 555명. 헬기 121대. 배 169척으로 우리아이들을 구출하고 있다고 거짓말 했습니다.

Tulipofika saa 5:30 katika ukumbi wa michezo wa Jindo ambapo ni kituo cha dharura, hakukuwa na mfanyakazi ambaye alikuwa na wajibu wa kuwaambia watu nini kinaendelea. Hakukuwa hata na kituo cha udhibiti […] Sisi tulitembelea eneo la ajali jana. Timu ya kuwaokoa ilikuwa chini ya watu 200 Kulikuwa na helikopta mbili tu, mashua mbili baharini, mashua mbili za walinzi wa pwani, mashua sita ya vikosi maalum.. Na watu wanane wa timu ya uokoaji wamefanya zoezi la kuokoa. Hata hivyo, Makao Makuu ya maafa yamesema uongo kwetu sisi kwamba wao waliwapeleka wanachama 555 wa uokoaji, helikopta 121 na mashua 169.

**Ripoti zaidi itafuatilia kuhusu maafa.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.