Pamoja na maonyo, kufuata mkumbo wa Siku ya Wajinga kungesababisha hukumu ya moto wa milele kwa kuwa Waislamu hawapaswi kudanganya, watumiaji wengi wa mtandaoni Uarabuni kote, waliamua kuzikosoa serikali zao siku hii.
Kutoka Saudi Arabia, Abdelrahman Al Kanhal anatania:
#كذبة_إبريل [2]
مشروعي الملك عبدالله لتطوير القضاء وتطوير التعليم
— عبدالرحمن الكنهل (@A_Alkanhal) April 1, 2014 [3]
King Abdulla amekubali mradi mpya wa kuendeleza mahakama na elimu
Na anaongeza:
الدولة تتخذ قرار تاريخي باتخاذ مواقف جادة لوقف الفوضى المرورية
#كذبة_إبريل [2]
— عبدالرحمن الكنهل (@A_Alkanhal) April 1, 2014 [4]
Nchi hiyo ya kifalme imechukua hatua madhubuti kumaliza tatizo la msongamano wa magari barabarani
Na akikumbushia kuzuiwa kwa wanawake kuendesha magari nchini humo, anaendelea kuandika:
#كذبة_إبريل [2]
المجتمع وحده يقرر حق المرأة في قيادة السيارة .. ولا نمنع قيادتها ولكننا نسجنها بسبب ارادة المجتمع الرافض
— عبدالرحمن الكنهل (@A_Alkanhal) April 1, 2014 [5]
Jamii yenyewe ndiyo yenye kuamua ikiwa ni haki kwa wanawake kuendesha ama la. Na hatuwapingi wanawake kuendesha ila tu kuwapeleka jela kama wataendesha kitendo kilicho kinyume na matakwa ya jamii
Wakati huo huo, Mmsri Adham Morad anadanganya kuhusu kutudi kwa Rais Mohamed Morsi kiongozi wa Muslim Brotherhood aliyeng'olewa madarakani hivi karibuni:
#كذبة_إبريل [2] موورسي راجع ههههه
— adham morad (@adham_morad) April 1, 2014 [6]
Morsi amerudi!!
Na, bado nchini Misri, Adilovic ana matamanio yake ya kimawazo. Anatwiti:
الحكومة المصرية تقرر رفع الأجور.. و زيادة الدعم.. و زيادة ميزانية التعليم والصحة.. وتوفير العيش والحرية والعداله الإجتماعيه
#كذبة_إبريل [2]
— Adilovic (@adilovic4a) April 1, 2014 [7]
Serikali ya Misri imeamua kuongeza mishahara, ruzuku, imeongeza bajeti ya huduma za elimu na afya na kuwapa wa-Misri maisha bora, uhuru na haki za kiraia
Kutoka Bahrain, Ammar Al Aradi, anawtiti mfululizo wa utani wa Siku ya Wajinga, ambao watu wengine walidhani ni kweli. Anabainisha:
Ok apparently some ppl are taking my last few tweets too seriously. It's first of April. Let's stop before someone gets in trouble lol.
— ammaro (@ammar456) April 1, 2014 [8]
Huu ni mmoja wa utani wake:
#Kuwait [9] considering legalizing hashish for medical uses after studies show more than 60% of the youth in the country already use it.
— ammaro (@ammar456) April 1, 2014 [10]
Kuwait imehalalisha mirungi kwa ajili ya matumizi ya kitabibu baada ya ushahidi kuonyesha kuwa zaidi ya asilimia 60 ya vijana nchini humo tayari wanaitumia
Tukirudi nchini Saudi Arabia, Ahmed Al Maani anahitimisha:
سيكون هذا الأمر مرهقاً للعرب لأنه لا يوجد شيء غير اعتيادي يمارسونه في هذا الشهر..
#كذبة_إبريل [2]
— احمد المعني (@rhal84) April 1, 2014 [11]
Siku ya wajinga Duniani itakuwa inachosha tu kwa Waarabu kwa sababu haina lolote lisilofanywa na Waarabu siku nyingine