
Utepe wa njano ukiwa umefungwa katika mtaa wa Seoul kwa matarajio ya muujiza wa janga la kivuko cha Sewol. Picha na Lee Yoo Eun.
Zimetimia siku 14 tangu kivuko cha Korea Kusini kizame kikiwa na abiria mamia kadhaa. Mpaka sasa, watu wapatao 205 wamethibitishwa kupoteza maisha, na wnegine 97 bado hawajulikani walipo.
Nahodha na wafanyakazi wote wa kivuko wote wamewekwa ndani. Waziri Mkuu Chung Hong-won tayari amejiuzulu kufuatia serikali kushutumiwa kuwa ilichelewa kuchukua hatua kukabiliana na janga hilo. Watu watatu kutoka kwenye ofisi ya Incheon ya Chama cha Usafiri wa Majini cha Korea nao wamekamatwa kwa tuhuma za kuharibu ushahidi.
Wakati taarifa zaidi kuhusu uzembe wa serikali ya Korea Kusini katika kushughulikia ajali hiyo zimepatikana, hasira za wananchi zimeendelea kuongezeka.
Kwenye mtandao, watumiaji wa intaneti wamezilaumu mamlaka za serikali na vyombo vya habari kwa kuendelea ‘kuimba’ visingizio vinavyotolewa na serikali:
위기관리 능력이 전혀 없는 정부의 무능과 거짓, 한술 더 떠서 거짓말만 해대는 미친언론에 분노한 피해자 가족들… 세월호 참사에서 이 나라의 밑바닥이 드러나고 있다. #뉴스타파 pic.twitter.com/I5010osha0
— 미권스 (@afc_4565) April 21, 2014
Mbinu mbovu za kukabiliana na majanga, udhaifu na uongo, na vyombo vya habari vinavyoendelea kudanganya mfululizo…Yote haya yameziumiza familia. Katika ajali hii ya kivuko cha Sewol, udhaifu wa serikali hii umefunuliwa.
뉴스에서 대통령이 사라졌다. 정부당국의 말실수, 집계누락 등 수많은 실책의 최종 책임자가 제일 먼저 언론에서 사라져버림. 마치 좌초한 세월호에서 선장이 제일 먼저 도망친 것처럼.
— 루나 (@fakemommy) April 20, 2014
Rais haonekani kwenye taarifa za habari. Madudu ya idara za serikali na makosa mengi na kushindwa kwa serikali havionekani kwenye taarifa za habari. Kama ilivyotokea kwenye kuzama kwa kivuko cha Sewol, nahodha wa meli alikimbia.
언론은 세월호 침몰 현장에 장비가 들어간 장면과 전문가들이 구조에 참여한 소식을 보여준다 언론만 보면 구조작업은 활발하다 하지만 현장에서 초기에 구조된 사람 외에 추가로 구조된 사람들은 없다 결과물은 없고 언론은 떠들고..언론보도와 현장은 전혀 다르다
— 임중수 (@js8088hb) April 19, 2014
Vyombo vya habari vinaonyesha video inayoonesha vifaa vilivyookolewa kutoka kwenye eneo la ajali ya kivuko hicho na vipande vya video zilizotengenezwa na wataalamu wakati wa zoezi la ukoaji. Inaonekana zoezi hilo linaendelea kwa ufanisi -kama tunategemea kupata habari kupitia vyombo vya habari pekee. Hata hivyo, hakuna wahanga wengine ukiacha wale waliokuwa wameokolewa katika eneo la ajali. Hakuna maendeleo, lakini vyombo vya habari vinaendelea kupiga porojo. Eneo hasa ilikotokea ajali ni tofauti na lile linaloonyeshwa na vyombo vya habari.
Hasira imechochewa zaidi na wanasiasa wanaoonekana kutumia tukio hilo kisiasa.
Mbunge wa chama tawala cha Saeunri yuko kikaangoni kwa kumtuhumu kimakosa mzazi wa mmoja wa wahanga wa ajali hiyo [ko] kuwa mtu asiyehusika ‘anayetaka kuchochea tu hasira dhidi ya serikali’. Mbunge huyo baadae alieleza kwamba alikuwa amepotoshwa na picha bandia zilizokuwa zinasambaa mtandaoni.
Polizi hivi sasa wanamchunguza mwandishi [ko] aliyeandika kwenye mtandao wa Facebook kwamba “Janga la kivuko cha Sewol ni tukio lililotengenezwa na vibaraka wa Korea Kaskazini wanaotaka kutengeneza mazingira ya hali ya sintofahamu na tahayaruki katika jamii ya Korea Kusini. ”
이제 국민을 좌빨에서 종북세력으로 몰아 간첩만들기는 일상화 됐다.수틀리면 개나 소나 종북,간첩을 외치는 이 어이없는 상황.세월호 인명구조에 한가닥 희망을 걸고 있는 분들은 이미 유리심장이다.작은상처에도 쉽게 상처받고 깨질 위험한 상황이니 말조심들해라
— 수연낙명(隨緣樂命) 안녕하지 못합니다 (@kriskimera) April 22, 2014
Sasa mbinu za kuwaita watu “wakomusnisti wekundu” na “Vibaraka wa [Korea] Kaskazini” limekuwa jambo la kawaida siku hizi. Hali hii inaudhi sana. Kila mmoja anamtuhumu mwenzake kuwa ni “Kibaraka wa kaskazini” au “Shushushu wa Korea Kaskazini” kila panapokuwa na hali ya kutokuelewana. Watu wale ambao bado hawajakata tamaa na zoezi la uokoaji linaloendelea, watu hao ambao wako katika wakati mgumu wanaweza kuumizwa kirahisi na matamshi ya namna hiyo. Tuangalie kile tunachokisema.
세월호로 온 나라가 슬픔에 잠기고, 정부의 무능을 비판하는 소리가 높아지자~여기에도 종북놀이를 해 대는 집권당과 그 지지자들을 보면, 나라가 이렇게 밖에 될수 없슴을 절감케 한다. 모든 잘못을 종북으로 덮는 지배층을 바꾸지 않으면 우린 답이 없다.
— 쟝고 (@shsh7600) April 22, 2014
Wakati nchi yote imezizima na kukata tamaa na kukaongezeka sauti za watu wanaoikosoa serikali, chama tawala na wafuasi wake wameanza kutengeneza propaganda ya “Vibaraka wa Kaskazini”. Mazingira haya yamenifanya vifikiri kuhusu kile kilichoifanya nchi yetu iingie kwenye matatizo. Kama hatuwezi kubadili uongozi unaofunika udhaifu wake kwa mbinu za eti ‘Ukibaraka wa Kaskazini’, basi hatuna jawabu.