Magonjwa ya Afya ya Akili Hayapewi Kipaumbele Nchini Cambodia

Akiandika kwa niaba ya Southeast Asia Globe, Denise Hruby aliripoti jinsi wagonjwa wa akili katika maeneo mengi ya vijijini vya Cambodia wanavyofanyiwa:

…Wagonjwa wa akili bado hutibiwa na waganga wa jadi, ambao lengo lao ni kuwatoa pepo wabaya kwa kuchoma ngozi, au kwa wafanyakazi wasio na ujuzi wa chumba kimoja cha kliniki za afya ambao huwapa kila kitu kutoka vidonge vya dawa ya kupunguza maumivu hadi dawa ya kikohozi.

Kwa mujibu wa msemaji wa serikali Phay Siphan, afya ya akili si kipaumbele:

Serikali imeipa kipaumbele afya ya uzazi na ugonjwa wa malaria. Kwa afya ya akili, najua kwamba serikali inazo fedha za kugharamia, lakini sisi tu maskini.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.