- Global Voices in Swahili - https://sw.globalvoices.org -

Pigia kura Blogu ya Kenya Uipendayo

Mada za Habari: Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Kenya, Uandishi wa Habari za Kiraia

Zoezi la upigaji kura limeanza [1] kwa ajili ya Tuzo za Blogu nchini Kenya kwa mwaka 2014:

Chama cha wanablogu wa Kenya (BAKE) hii leo [3 Machi 2013] kilizindua zoezi la kupendekeza majina ya wawaniaji wa tuzo hizo za wanablogu wa Kenya mwaka huu. Tuzo hizo hutolewa kwa wanablogu waandikao maudhui muhimu na yanayotolewa kwa ubunifu na muundo bunifu.

Wateuzi walichaguliwa na jopo la majaji lililohusisha wanablogu na waaandishi kutoka vyombo vya habari.

Kutolewa kwa orodha ya wateuzi huashiria kuanza kwa zoezi la kupiga kura kwa tuzo hizo.

Kupiga kura kutaanza kuanzia Machi 3, 2014 na kumalizika Aprili 30 2014

Unaweza kupigia kura blogu yako uipendayo kupitia tovuti ya www.blogawards.co.ke/vote