Inataarifiwa kuwa watu 500,000 wameshindwa kutoka katika vijiji wanavyoishi huku wakikosa huduma ya umeme, nishati ya gesi pamoja na maji [1] hali iliyotokana na kutanda kwa theluji mwisho wa wiki hii Kaskazini mwa nchi ya Iran katika majimbo ya, Gilan [2] na Mazandaran [3].
Afisa mmoja alisema kuwa hili ni anguko kubwa la theluji ambalo halikuwahi kutokea kwa miaka 50 iliyopita [4]. Hadi sasa, maelfu ya watu wameshaokolewa na kupelekwa kwenye makazi ya muda au kulazwa hospitalini.
ZA1-1RA alitwiti [5]:
من ازین باباتم خیالم از خونواده جمه که می دونم اندازه چن ماه برنج دارن #برف [6] #شمال [7] :|
— ZA1-1RA (@zara_esm) Tar 3 Februari, 2014 [8]
Sina shaka na familia yangu, wana hifadhi ya kutosha ya mchele kwa matumizi ya miezi kadhaa.
Farshad Faryabi alitwiti [9]:
فکر کنم #وزیرخارجه [10] #سوئد [11] برنگرده از ایران چون الان #برف [6] و سرما تو #ایران [12] بیشتر از سوئد شده :)
— Farshid Faryabi (@F_Faryabi) Tar 3 Februari, 2014 [13]
Waziri wa mambo ya nje wa Swiden, Carl Blidt, [aliyeko safarini nchini Iran] hataweza kurudi Swiden kutoka na hali tete ya theluji nchini Iran.
Soheila Sadegh alitwiti [14]:
به علت بارش برف در شرق #گيلان [15]، یک مدرسه ابتدایی بدلیل فرسودگی تخریب شد #آموزشپرورش [16] #مدارس [17] #دانشآموز [18] #معلم [19] #مازندران [20] #رشت [21] #گرگان [22] #اردبيل [23]
— soheila sadegh (@Soheila_Sadegh) tar 3Februari, 2014 [24]
Theluji nzito yaharibu vibaya shule huko Gilan.
Maysam Bizar alitwiti [25]:
شهروند #مازندرانی [26]: بخاطر #برف [6] 6 عدد آب معدنی کوچک 3 هزار تومانی را خریدیم 12 هزار تومان. خودمون به خودمون رحم نمیکنیم از دشمن انتظار داریم؟
— Maysam Bizar (@M_Bizar) tar 3 Februari, 2014 [27]
Gharama ya maji ya chupa yalipanda mara nne zaidi ya bei ya kawaida katika kipindi cha tatizo la theluji. Kama hatuwezi kujihurumia, labda cha kufanya ni kutegemea maadui?
Mozdeh A alitwiti [28]:
هر چی برا بقیه دنیا نعمته واسه ایرانی جماعت نکبته #برف [6]
— mozhdeh A (@MozhdehT) tar 3 Februari, 2014 [29]
Kilicho na Baraka kwa wengine, kwetu ni laana.
Saham Borghani mwezi uliopita (tar 10 Januari) aliweka [30] picha ya chain a barafu.
#برف [6] و #چای [31] pic.twitter.com/6phbpubCjJ [32]
— saham Boorghani (@sahamedin) tar 10 Januari, 2014 [33]