PICHA: Vyama vya Wafanyakazi na Asasi za Kiraia Vyaandaa Mgomo

Huku ukiwa umepangiliwa ufanyike mwanzo wa kipindi cha pili cha Rais Park Geun-hye madarakani, takribani wa-Korea elfu 40 (polisi wanadai ni elfu 15) walifanya mgomo nchini kote. Mgomo huo, ulipangwa na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini Korea, ukiwa na wito wa kusitishwa kwa kudhibitiwa kwa vyama vya wafanyakazi, hatua ya serikali kubinafsisha sekta ya umma na kufunikwa skandali ya wizi wa kura katika uchaguzi wa rais. Mwandishi wa habari za kiraia anayeheshimika Mongu alitwiti picha ya maandamano (imewekwa hapa chini). Picha zaidi zinaweza kupatikana kwenye ukurasa wa Facebook wa chama cha wafanyakazi [ko].

Mgomo mkubwa, kwenye Ukumbi wa Seoul City Hall Plaza. Ulijaa vilivyo.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.