Wasomaji wa kimataifa wanaofuatilia masuala ya Korea Kaskazini labda wangekutana angalau mara moja na picha hii maarufu ya rasi ya Korea [1] kutoka Shirika la Anga la Marekani (NASA) kuonesha tofauti kubwa ya taa zinazoangaza usiku kwenye nchi hizo mbili za Korea. NASA hatimaye walihuisha picha zao za Satelaiti [2] na ‘ina mwonekano mzuri kuliko picha ya zamani ya NASA’, inaandika blogu ya Teknolojia ya Korea Kusini [3]. Blogu hiyo pia inatambulisha toleo la video la picha hiyo [4] linaloonyesha Korea Kaskazini katika mukhtadha wa eneo lote la Asia Kaskazini.
Picha Mpya ya Korea Kaskazini ya Shirika la Anga la Marekani
· Imeandikwa na Lee Yoo Eun Imetafsiriwa na Mghosya
Mada za Habari: Asia Mashariki, Korea Kaskazini, Korea Kusini, Mahusiano ya Kimataifa, Sayansi, Teknolojia, Uandishi wa Habari za Kiraia, Upiga Picha