Picha Mpya ya Korea Kaskazini ya Shirika la Anga la Marekani

Wasomaji wa kimataifa wanaofuatilia masuala ya Korea Kaskazini labda wangekutana angalau mara moja na picha hii maarufu ya rasi ya Korea kutoka Shirika la Anga la Marekani (NASA) kuonesha tofauti kubwa ya taa zinazoangaza usiku kwenye nchi hizo mbili za Korea. NASA hatimaye walihuisha picha zao za Satelaiti na ‘ina mwonekano mzuri kuliko picha ya zamani ya NASA’, inaandika blogu ya Teknolojia ya Korea Kusini. Blogu hiyo pia inatambulisha toleo la video la picha hiyo linaloonyesha  Korea Kaskazini katika mukhtadha wa eneo lote la Asia Kaskazini. 

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.