Rais wa serikali ya mpito ya Misri, Adly Mansour atoa amri ya Rais ya kumpandisha cheo Jenerali Abdel Fattah El-Sissi, ambaye ni waziri wa ulinzi kuwa Jemadari Mkuu. Hii ni nafasi ya juu kabisa katika jeshi la Misri
Upandishwaji cheo huu umezua mjadala mkubwa katika mitandao ya intaneti ambapo watu wengi wanajiuliza kama ndio njia ya Sissi kugombea urais unaotarijiwa kufanyika mwisho wa mwezi Aprili.
Adam Makary katika ukurasa wa Twita aandika:
Reminder – Sisi #Egypt [1]'s alikuwa ni waziri wa ulinzi wa kwanza ambaye hakustahili kupewa nafasi kuu kabisa ya Jemadari Mkuu. Kwa sasa tayari ameshatunukiwa.
— آدم مكاري (@adamakary) tarehe 27 Januari, 2014 [2]
Louisa Loveluck atoa angalizo:
Field Marshal Sisi's Ukurasa wa Wikipedia tayari umeshaboreshwa .
— Louisa Loveluck (@leloveluck) tarehe 27 Januari, 2014 [3]
Pia, Ahmed Abrass anafafanua maana ya cheo cha Jemadari Mkuu [ar]:
رتبه المشير ترجمتها بالانجليزيه فيلد مارشال قائد ميدان حرب و هي تمنح للعسكريين اللي قادوا جيوش لانتصارات مبهره
— Ahmed (@Ahmed_Abrass) tarehe 27 Januari, 2014 [4]
” Kwa kiingereza, Jemadari Mkuu ina maana kuwa mtu Fulani aliyewangoza wanajeshi vitani na akapata ushindi mkubwa .”
Kwa El Siss, hili si jambo la yeye kulitilia maanani. Hata hivyo, inaonekana kuwa kuwa Jemadari Mkuu siyo kigezo cha muhimu katika jeshi la Misri na hata hivyo Meja Jenerali huyu mstaafu alikuwa na vigezo vyote vya kumfanya kuwa Jemadari Mkuu .
Nervana Mahmoud afafanua:
This arabic link say: " Kushiriki katika vita siyo kigezo cha kumpandisha mtu cheo hadi kuwa Jemadari Mkuu." http://t.co/pi9dbLS4RX [5] kabisa! #Egypt [1]
— Nervana Mahmoud (@Nervana_1) tarehe 27 Januari, 2014 [6]
Bel Trew athibitisha kuwa:
Abdel-Fattah Sisi alikuwa na vigezo vyote vya kuwa Jemadari Mkuu, doesn't need combat experience say sources #Egypt [1] http://t.co/5tmFOlQPPS [7]
— Bel Trew – بل ترو (@Beltrew) tarehe 27 Januari, 2014 [8]
Na Egyptian Streets asema:
Chanzo cha Serikali: Kupandishwa cheo kwa Al-Sisi kumekuwa na lengo la kutambua kazi aliyoifanya kwa miezi kadhaa iliyopita. #Egypt [1]
— Egyptian Streets (@EgyptianStreets) tarehe 27 Januari, 2014 [9]
Watumiaji wengi wa mtandao wameonesha kushangazwa na waziwazi kuchukizwa na habari hii.
Katika mtandao wa kijamii wa Facebook, Mina Labib auliza [ar]:
يتكافؤه على ايه ؟؟ علي إنفجارات ؟؟!!
Anatunukiwa hasa kwa lipi alilolifanya? Kuhusu milipuko iliyotokea?
Januari 24, Misri ilikabiliwa na mfululizo [10] wa milipuko iliyoua watu sita na wengine 70 walijeruhiwa huko Cairo.
Baadhi ya watu wanaona kuwa, kupandishwa cheo huku ni namna ya ya haraka ya Sissi kuelekea kugombea Urais. Nervana Mahmoud aandika:
Kupandishwa cheo kwa Sisi ni ishara ya karibu sana ya kuachia madaraka. Hivi ndivyo mambo yalivyozoeleka kufanyika nchini Misri kwa miongo mingi. #sigh [11]
— Nervana Mahmoud (@Nervana_1) tarehe 27 Januari, 2014 [12]
Egyptian Streets adds:
BREAKING: Reports indicate Al-Sisi meeting with military leaders to plan his nomination for Presidency, likely to resign. #Egypt [1]
— Egyptian Streets (@EgyptianStreets) tarehe 27 Januari, 2014 [13]
Na pia, mwanahabari Patrick Kingsley anafafanua:
Ni punde tu niliongea na afisa mkubwa wa jeshi ambaye alitanabaisha kuwa #Sisi [14] angepaswa kuachia ngazi kama atagombea Urais. Lakini, hakuweka wazi kupandishwa cheo kwa Sissi kulikuwa na maana gani.
— Patrick Kingsley (@PatrickKingsley) tarehe 27 Januari, 2014 [15]
Inaonekana kuwa kugombea Urais siyo sababu pekee ya kupandishwa cheo hiki. Tarik Salama atwiti:
Sisi kupandishwa cheo kama Jemadari Mkuu ni kwa minajili ya kuongezewa mshahara. Kama Rais mtarajiwa na ikizingatiwa na ukomo wa mshahara wa Rais uliopo kwenye katiba, upandishwaji huu wa cheo ni kama namna ya kumhakikishia mshahara wa ziada.
— Tarik Salama (@tariksalama) tarehe 27 Januari, 2014 [16]
Basil Al Dabh anaongeza:
Uipate pensheni hiyo. #recession [17]
— Basil الضبع (@basildabh) tarehe 27 Januari, 2014 [18]
Katika kipindi cha taharuki na kutokujali uhuru wa mtu, baadhi ya watu wanaokuwa hii ni hatua nyingine kuelekea kuheshimu watu kama Mungu wao na kuwapenda, mfumo ambao viongozi wa Misri wamekuwa wakiusimamia.
Zack Gold afafanua:
kwa hali ilivyo, ninafikiri kuwa, cheo kitakachofuatia ni cha " Mungu Jua."
— Zack Gold (@ZLGold) tarehe 27 Januari, 2014 [19]
Gr33ndata akiweka kikaragosi:
Viva Alcazar pic.twitter.com/lUJfgpNde3 [20]
— Tarek Amr (@gr33ndata) tarehe 27 Januari, 2014 [21]