Kiongozi wa Upinzani Nchini Venezuela Leopoldo López Ajisalimisha Serikalini

Kiongozi wa Upinzani nchini Venezuela Leopoldo López amejisalimisha mwenyewe kwa Vikosi vya Polisi, kama alivyokuwa ametangaza angefanya kwenye video [es] hiyo hapo juu.

López, kiongozi wa chama cha Voluntad Popular, alitakiwa  kujisalimisha kwa agizo la mahakama jijini Caracas kwa kutuhumiwa kuhusika na makosa ya jinai yanayohusiana na maandamano  yanayoendelea nchini Venezuela.    

Maandamano makubwa ambayo López alijisalimisha siku ya Februari 18 yalikuwa yalikuwa ya amani, na wafuasi wake walipiga kelele [es]  kumwuunga mkono. Twiti ifuatayo ina mkusanyiko wa picha za maandamano na pia za tukio la López kujisalimisha kwenye mamlaka za serikali jijini Caracas: 

Venezuela- Maandamano ya Februari 18

Video hii [es] ilipigwa wakati López akijisalimisha: 

Na kwenye video hii [es] unaweza kumsikia López akihutubia umati wa waandamanaji akiwa kwenye gari ya polisi lililokuwa likilindwa kwa silaha na ambalo lingempeleka kwenye Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali nchini Venezuela.

Mpaka toleo la lugha ya Kihispania la posti hii linaandikwa, watu walikuwa bado wako mitaani wakiandamana[es].

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.