Habari kutoka 27 Novemba 2013
Onesho la Mitindo Nchini Japan na Kauli Mbiu ya Kusitishwa kwa Matumizi ya Nguvu Dhidi ya Wanawake
Umoja wa Wanawake wa Asia, shirika lisilo la kimaslahi linaloshughulika na haki za wanawake linaratibu onesho la mitindo linalobeba ujumbe wa Mtindo wa Kukabiliana na Mfumo Kandamizi kwa lengo la kuvuta hisia za watu kuhusiana na suala la matumizi ya nguvu dhidi ya Wanawake.
Mkusanyiko wa Makala za Kuvuliwa Madaraka kwa Mbunge Maarufu Nchini Tanzania
Ben Taylor aweka mkusanyiko wa makala zinazohusiana na kuvuliwa madaraka kwa Zitto Kabwe,mbunge maarufu na kijana wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema. Zitto: […] alivuliwa nyadhifa zote rasmi na viongozi wakuu wa chama mapema siku ya ijumaa asubuhi. Zitto Kabwe hatakuwa tena Naibu katibu Mkuu wa chama wala...
Wanasayansi Kutoka Duniani Kote Wakusanyika Nchini Brazil
Jukwaa la Sayansi Duniani (WSF) linajumuisha mamia ya wanasayansi kutoka duniani kote wiki hii nchini Brazil, kujadili wajibu wao katika karne ya 21 na kusisitiza umuhimu wa ushauri wa kisayansi katika maamuzi ya kisiasa na kiuchumi. Brazil imekuwa mwenyeji wa matukio kadhaa ya kujadili kuondoa umaskini na maendeleo endelevu kutoka...
VIDEO: Serikali Yaharibu Misikiti Nchini Angola
Uharibifu wa misikiti isiyopungua 11 katika miezi miwili iliyopita nchini Angola imechochea athari ya hasira kwenye mtandao. Kwa mujibu wa Voz da América [pt], Mamlaka ya Angola ilisema kuwa sababu ya uharibifu ni ujenzi kinyume cha sheria na ripoti&nyingine kuongeza kwamba mchakato wa kuhalalisha Uislamu na dini nyingine katika nchi haijawahi...
Iran: Mwanablogu Aliyefungwa Jela Ahitaji Huduma ya Matibabu ya Haraka
Mwanablogu aliyefungwa jela,Hossein Ronaghi Maleki anahitaji huduma ya matibabu ya haraka. Alihukumiwa kifungo cha jela cha miaka 15. Laleh alitwiti Mwanaharakati aliyefungwa jela Hossein Ronaghi yuko katika hali mbaya ya afya, kuvimba figo -(moja haifanyi kazi), kibofu cha mkojo na ugonjwa wa kibofu #Iran #Iranelection — Lalehلاله (@Lalehsr) Novemba 25,...