Wali Unaonata Haufai kwa Watoto, Akina Mama Waambiwa

@LaotianMama anawakumbusha akina mama wa Lao kutokuwalisha watoto wenye njaa wali unaonata ambao ni chakula cha asili kwao.

Wali unaonata kwa watoto wachanga ni sawa na punje za wali katika utamaduni wa ki-Magharibi. Wazo ni lile lile kuwa kuwapa watoto wachanga chakula kigumu kutawashibisha. Kwa hiyo, kuwaanzishia watoto wachanga chakula ambacho ni kama hakina virutubisho zaidi ya kushibisha tu inaweza kuwa hatari kwa mfumo wa chakula ambao unakuwa bado haujaimarika vilivyo na kunaweza kusababisha matatizo ya mtoto kupata magonjwa yanayotokana na mwili wake “kukataa” chakula [allergies], anaweza kupata udumavu, na hata shida ya kutokunyonya ipasavyo.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.