Karibu matukio 500 ya moto wa msituni yalirekodiwa katika kisiwa cha Sumatra mwezi Agosti matukio ambayo yalisababisha vumbi nene kutimka angani Riau nchini Indonesia na hata katika baadhi ya maeneo ya Malaysia. Uchomaji wa misitu ni unasemekana kusababishwa na shughuli za kilimo cha mashamba makubwa ya mafuta ya mawese, makubaliano ya uuzaji wa kuni, na mashamba ya mashapo. Shule kadhaa zilifungwa katika jimbo la Riau wakati wa vumbi hilo baya lilipoonekana tena wiki iliyopita.
Vumbi linalosababishwa na uchafuzi wa mazingira ni tatizo la mara kwa mara katika eneo hilo linalosababishwa zaidi na matukio ya moto wa msituni nchini Indonesia. Mwezi Juni, vumbi nene kiliifunika Singapore na maeneo mengi nchini Malaysia.

Maeneo yanayoonesha matukio ya moto wa msituni jimboni Riau, Indonesia. Maeneo yenye rangi ya manjano ni mashamba makubwa ya mawese. Picha ya Eyes on the Forest [Macho Misituni].
Kwenye mtandao wa Twita, Wa-Indonesia walionyesha wasiwasi wao juu ya kurejea tena kwa vumbi hilo huko Sumatra.
If Indonesia Prez dtg, pls tell Msian palm oil owners in Sumatra to burn more fires so tht SBY can see with his own eyes what Haze is.
— Dr Wan Norashikin (@drshikin) August 31, 2013
Kama Rais wa Indonesia [anayefahamika kwa kifupi kama SBY, Susilo Bambang Yudhoyono, waambieni wamiliki wa mashamba ya mawese wachome moto zaidi ili [Rais SBY] aone kwa macho yake vumbi hili linafananaje
#haze #Sumatra land burning bad for 2 days in #Medan, left a layer of black dust on my motorcycle in 8 hours #health #environment #Indonesia
— SumatraEEC (@SumatraEEC) August 27, 2013
Ardhi inateketea vibaya kwa moto kwa siku mbili huko Medan, imeacha vumbi jeusi kwenye pikipiki yangu kwa masaa nane tu
Huko Penang, vumbi hilo liliathiri wakazi wengi. Kwa bahati nzuri, vumbi lilikuwa tayari kimekwisha mwishoni mwa wiki iliyopita.
Haze is stopping me from jogging ):
— June (@SScarsorrow) August 29, 2013
Vumbi hili linanizuia kufanya mazoezi ya kukimbia kimbia
Finally, no more haze. Yeay. I can finally see the sunrise. Alhamdulillah. Morning suria
— Ameera Nadia Shafiee (@ameeranadia90) August 30, 2013
Hatimaye, hakuna vumbi zaidi. Safi. Hatimaye naweza kuona mawio ya jua. Alhamdulillah. Asubuhi njema