Kubusiana Kwenye Mitaa ya Misri

Picha inayosambazwa katika mtandao wa Facebook inayowaonyesha vijana wawili raia wa Misri wakibusiana barabarani iliibua hasira na wengine kuipenda. Ilitolewa na Ahmed ElGohary, mtangazaji aliyepingwa kwa ‘kukosa utu uzima’ kwa sababu ya kuweka picha ya jinsi hiyo. Wengine walisifu uzuri wa picha hiyo na tafsiri yake kwa mapinduzi ya kiutamaduni.

Two young lovers kiss on the street in Egypt, shared by Ahmed ElGohary  https://www.facebook.com/photo.php?fbid=10151429894938231&set=a.10151035748418231.432064.669983230&type=1&theater

Vijana wawili wakibusiana barabarani nchini Misri. Picha: Ahmed ElGohary http://tinyurl.com/l3rozz9

Kuonyesha mapenzi hadharanini si jambo linalokubalika nchini Misri, na sheria ya kuzuia kukosa maadili hadharani inaweza kutumika kuwashitaki wale wanaothubutu kuonyesha mapenzi hadharani au kunywa pombe katika mitaa.

Sambamba na picha, ElGohary aliweka mashairi ya wimbo wa Youssra El Hawary uitwao On The Street [Mtaani]. El Hawary mwimbaji huru chipukizi na nyimbo zake zimeonyesha mafanikio kwenye mtandao wa youtube. Mashairi ya On The Street yansema:

Baadhi ya watu kuwalaani wengine, kuua kila mmoja kwenye mitaani,
Watu wengine hulaaniana, huuana kwenye sakafu za mitaani,
Watu wengine huuza heshima zao mitaani,
Lakini ingekuwa kashfa ya kweli kama siku moja tutasahau na kubusiana kwenye mitaani!

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.