Mwana-Habari Menna Alaa Ashambuliwa na Wafuasi wa Morsi

Mwanablogu na mwanahabari wa video Menna Alaa leo hii ameshambuliwa na waandamanaji wenye hasira wanaomwunga mkono Morsi. Mwanablogu huyo ameweka ushuhuda wake kwa lugha ya kiingereza kwenye makala hii iliyo katika blogu inayokusanya matukio nchini Misri iitwayo Egyptian Chronicles. Anaandika:

Kofi nililopigwa usoni, alama iliyobaki usoni mwangu pamoja na kuibwa kwa kamera yangu hakutanizuia kuendelea kutoa habari. Ninatoa habari ya kile nikionacho na nitaendelea kuhabarisha pamoja na kuhatarisha maisha yangu. Ukweli ni kile kitakachonifanya niendelee kuipenda kazi yangu.

2 maoni

jiunge na Mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.