- Global Voices in Swahili - https://sw.globalvoices.org -

Barua ya Wazi ya Kushinikiza Kuachiwa Huru kwa Mwanasheria

Mada za Habari: Asia Mashariki, China, Haki za Binadamu, Sheria, Uandishi wa Habari za Kiraia

Mnamo Julai 23, 2013, zaidi ya raia 400 wa China wamesaini barua ya kushinikiza serikali ya China kumuachia huru Xu Zhiyong, ambaye ni mwanasheria mashuhuri na mpigania haki aliyekamatwa mnamo Julai 16 [1] baada ya kushinikiza kuachiwa kwa wanaharakati pamoja na kuratibu kampeni dhidi ya uovu unaofanywa na serikali. MRADI WA VYOMBO VYA MAWASILIANO WA CHINA (CHINA MEDIA PROJECT) ulitafsiri [2] barua hii kwenda katika lugha ya Kiingereza.