Habari kutoka 12 Julai 2013
Al Jazeera Yatuhumiwa Kutangaza “Habari za Upendeleo”
Al Jazeera iko kwenye wakati mgumu nchini Misri kwa kile kinachoelezwa na wengi kuwa ni "upendeleo" wake katika kutangaza habari zake wakati na baada ya kuondolewa madarakani kwa rais wa zamani wa Misri Mohamed Morsi mnamo Julai 4. Kituo hicho cha televisheni kilichopo nchini Qatar kinatuhumiwa kuegemea upande wa wafuasi wa Muslim Brotherhood na kimegeuka kuwa mdomo wa kikundi hicho.
Kuelekea uchaguzi wa Kambodia: Matumizi ya Mtandao wa Facebook
Watumiaji wa mtandao wa intaneti nchini Cambodia wanatumia mtandao wa Facebook kwa kiwango kikubwa katika kujadili, kuendesha midahalo na kushirikishana mambo mapya yanayohusu chaguzi za kitaifa zinazotarajiwa kufanyika tarehe 28 Julai, 2013. Wakati huohuo, vyama vya siasa pia vinatumia mtandao huu ulio maarufu zaidi katika kuwashawishi vijana wadogo wanaotarajiwa kupiga kura.