Kutokuwepo uwazi na weledi katika mchakato wa kumchagua mgombea, mbali na kufahamika nani hasa watachukua nafasi zinazogombewa kabla hata ya uchaguzi katika taasisi hiyo. Hizo zilikuwa baadhi ya sababu zilizotolewa na mwanaharakati wa haki za binadamu, Benilde Nhalivilo, wakati akijitoa rasmi kugombea nafasi kwenye Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Msumbiji [1][pt], chombo kinachohusika na kuandaa na kusimamia chaguzi nchini humo. Taarifa zaidi zinapatikana kwenye gazeti la A Verdade [2][pt].
Uchaguzi Tume ya Uchaguzi Msumbiji: Mwanaharakati Ajitoa Kugombea
· Imeandikwa na Thiana Biondo (en) imetafsiriwa na Thiana Biondo, Mghosya
Mada za Habari: Msumbiji, Siasa, Uandishi wa Habari za Kiraia, Uchaguzi, Utawala