Habari kutoka Mei, 2013
Mfululizo wa Tamthilia ya Runinga ya Nchini Tanzania
The Team Tanzania (Timu Tanzania) ni mfululizo wa Tamthilia ya Runinga yenye kuzungumzia: […] Bi. Wito, mwalimu mahiri wa somo la uraia, anaigeuza kabisa mitazamo ya vijana makinda watatu anapowauliza maswali mazito mfano “Wewe ni nani”? vijana wale wenye umri wa miaka 16, waliofahamiana vyema tangu wakikua. Katika kuingia katika...
Michoro ya Dar: Sanaa kwa Maendeleo Endelevu
Dar Sketches (Michoro ya Dar) ni sehemu ya mradi unaoanzia ngazi ya Mtaa jijini Dar Es Salaam, Tanzania ulioanzishwa na msanii na mchoraji Sarah Markes: Ni katika kuenzi urithi wa kitamaduni na wa sanaa ya ubunifu wa majengo kwa jiji la Dar Es Salaam sambamba na juhudi za kukuza uelewa...
TEDXSão Tomé: Mkutano Wanukia São Tomé na Príncipe
Uandikishaji wa awali kwa ajili ya mkutano wa TEDXSão Tomé umezinduliwa rasmi. Mkutano huo una kaulimbiu inayosema “Visiwa Vimeunganishwa : São Tomé + Príncipe = Áfrika Vimeunganishwa na Ulimwengu” na utafanyika tarehe 20 Juni. Wasemaji katika mkutano huo waliothibitishwa ni pamoja: Dynka Amorim, Ismael Sequeira, Profesa Robert Drewes na Aoaní...
China Yadhibiti Habari za Maandamano Yakupinga Kujenga Kiwanda cha Kemikali
Wakazi wa jiji la kusini magharibi mwa China liitwalo Kunming waliingia mtaani mnamo Mei 4, 2013 kupinga mpango wa kuzalisha kemikali zenye sumu karibu na makazi yao. Vyombo vya Habari vya serikali havikutangaza habari za maandamano hayo, na katika hali ya kushangaza wafuatiliaji wa mtandaoni wamefuta habari na picha zinazohusiana na maandamano hayo kwenye mtandao maarufu wa kijamii uitwao Sina Weibo tangu Mei 4, 2013.
Wagombea wa Urais katika Uchaguzi wa Madagaska
Habari Mpya: Hapa ni orodha kamili ya wagombea 49 [fr] wanaowania nafasi ya Urais katika uchauzi ujao. Orodha hiyo haina jina la rais wa sasa wa mpito. Siku ya mwisho ya kurudisha fomu kwa ajili ya kugombea Urais katika uchaguzi ujao ilikuwa tarehe 28 Aprili, na inavyoonekana ni wagombea wachache sana...
Maelfu ya Wafanyakazi Waandamana Barani Asia
Global Voices inayapitia kwa haraka maandamano ya Siku ya Wafanyakazi Mei Mosi kwenye nchi za Cambodia, Filipino, Indonesia na Singapore. Mikutano, ambayo iliandaliwa kudai haki za wafanyakazi na makundi mengine ya utetezi, yalifanyika kwa amani katika bara lote la Asia ya Kusini Mshariki.
Ethiopia: Mwanablogu Ahukumiwa Miaka 18 Jela kwa “Kuvunja Katiba”
Mnamo Mei 1, Mahakama Kuu ya Ethiopia ilitoa hukumu kali kwa mwandishi aliyeshinda tuzo Eskinder Nega, ambaye sasa atatumikia kifungo cha miaka 18 jela. Mohamed Keita wa Kamati ya Kuwalinda Waandishi anasema, “Kushitakiwa na hatimaye kutiwa hatiani kwa Eskinder na waandishi wengine ni dalili za utawala unaoogopa maoni ya raia wake.”
Wabunge wa Ukraine Wataka Utoaji Mimba Upigwe Marufuku Kisheria
Mapema mwezi Aprili, Wabunge watatu kutoka kambi ya Upinzani iitwayo“Svoboda” walipeleka mswada bungeni wenye lengo la kupiga marufuku utoaji mimba nchini Ukraine. Tetyana Bohdanova anataarifu mwitikio wa watumiaji wa mtandao kufuatia hatua hii ya Bunge la Ukraine.