Mei, 2013

Habari kutoka Mei, 2013

Mfululizo wa Tamthilia ya Runinga ya Nchini Tanzania

The Team Tanzania (Timu Tanzania) ni mfululizo wa Tamthilia ya Runinga yenye kuzungumzia: […] Bi. Wito, mwalimu mahiri wa somo la uraia, anaigeuza kabisa mitazamo ya vijana makinda watatu anapowauliza maswali mazito mfano “Wewe ni nani”? vijana wale wenye umri wa miaka 16, waliofahamiana vyema tangu wakikua. Katika kuingia katika...

TEDXSão Tomé: Mkutano Wanukia São Tomé na Príncipe

Uandikishaji wa awali kwa ajili ya mkutano wa TEDXSão Tomé umezinduliwa rasmi. Mkutano huo una kaulimbiu inayosema “Visiwa Vimeunganishwa : São Tomé + Príncipe = Áfrika Vimeunganishwa na Ulimwengu” na utafanyika tarehe 20 Juni. Wasemaji katika mkutano huo waliothibitishwa ni pamoja: Dynka Amorim, Ismael Sequeira, Profesa Robert Drewes na Aoaní...

China Yadhibiti Habari za Maandamano Yakupinga Kujenga Kiwanda cha Kemikali

  6 Mei 2013

Wakazi wa jiji la kusini magharibi mwa China liitwalo Kunming waliingia mtaani mnamo Mei 4, 2013 kupinga mpango wa kuzalisha kemikali zenye sumu karibu na makazi yao. Vyombo vya Habari vya serikali havikutangaza habari za maandamano hayo, na katika hali ya kushangaza wafuatiliaji wa mtandaoni wamefuta habari na picha zinazohusiana na maandamano hayo kwenye mtandao maarufu wa kijamii uitwao Sina Weibo tangu Mei 4, 2013.

Wagombea wa Urais katika Uchaguzi wa Madagaska

Habari Mpya:  Hapa ni orodha kamili ya wagombea 49 [fr] wanaowania nafasi ya Urais katika uchauzi ujao. Orodha hiyo haina jina la rais wa sasa wa mpito. Siku ya mwisho ya kurudisha fomu kwa ajili ya kugombea Urais katika uchaguzi ujao ilikuwa tarehe 28 Aprili, na inavyoonekana ni wagombea wachache sana...

Maelfu ya Wafanyakazi Waandamana Barani Asia

  4 Mei 2013

Global Voices inayapitia kwa haraka maandamano ya Siku ya Wafanyakazi Mei Mosi kwenye nchi za Cambodia, Filipino, Indonesia na Singapore. Mikutano, ambayo iliandaliwa kudai haki za wafanyakazi na makundi mengine ya utetezi, yalifanyika kwa amani katika bara lote la Asia ya Kusini Mshariki.

Ethiopia: Mwanablogu Ahukumiwa Miaka 18 Jela kwa “Kuvunja Katiba”

GV Utetezi  4 Mei 2013

Mnamo Mei 1, Mahakama Kuu ya Ethiopia ilitoa hukumu kali kwa mwandishi aliyeshinda tuzo Eskinder Nega, ambaye sasa atatumikia kifungo cha miaka 18 jela. Mohamed Keita wa Kamati ya Kuwalinda Waandishi anasema, “Kushitakiwa na hatimaye kutiwa hatiani kwa Eskinder na waandishi wengine ni dalili za utawala unaoogopa maoni ya raia wake.”