Januari 24, ni siku ambayo inategemewa kuwa ya kuzindua rasmi Hadithi [2], ambalo ni jukwaa la kuhifadhia [3] zana za bure za kitaaluma mjini Nairobi, Kenya. Wasomi mbalimbali na wadau wa mitandao watakusanyika pamoja kujadili upatikanaji wa zana huru za kitaaluma katika elimu ya juu nchini Kenya. Hadithi itasaidia kutafuta, kuona na kushusha makala kutoka katika taasisi za kitafiti duniani kote. Kujiandikisha kwa tukio hili, itafute Hadithi mtandaoni kupitia Facebook [4] na tovuti ya Eventbrite [5].
Jukwaa la Kiafrika Lenye Makala za Bure za Kitaaluma
· Imeandikwa na Laila Le Guen (en) imetafsiriwa na Lova Rakotomalala, Mghosya
Mada za Habari: Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Kenya, Elimu, Teknolojia, Uandishi wa Habari za Kiraia