Habari kutoka Agosti, 2012
Tanzania, Ethiopia: Meles Zenawi ‘Atuma Twiti’ Kutoka Kilindi cha Kaburi
"@zittokabwe tafadhali uwe bora kuliko mimi nilivyokuwa. Huku juu hakuna utani, tayari ninalipia makosa yangu." Twiti iliyotumwa na Waziri Mkuu wa Ethiopia Meles Zenawi baada ya kifo chake kwenda kwa Mbunge wa Tanzania Zitto Kabwe na kuibua mjadala mtandaoni.
Mauritania: Wafanyakazi wa Migodini Wapinga ‘Aina Mpya ya Utumwa’
Zaidi ya wafanyakazi 2,300 wako kwenye mgomo nchini Mauritania katika mji wa kaskazini wa Zouerat, jambo ambalo limesababisha kuzorota kwa maeneo mengine kumi ya Kampuni la Taifa la Madini na Viwanda, huku kazi zikiwa kwenye mvurugiko mkubwa. Madai yamejikita katika suala zima la maslahi bora ya wafanyakazi.
Saudi Arabia: Mwanaharakati Reema Al Joresh Atiwa Kizuizini katika Sikukuu ya Idi
"Hamjambo? Polisi wamenikamata mimi na watoto wangu." - Reema Al Joresh, mke wa mfungwa ambaye amekuwa kizuizini kwa miaka nane bila kufunguliwa mashtaka, alikuwa akielekea msikitini ili kutoa zawazi 500 pamoja na barua ya kueneza taarifa kuhusu itiaji nguvuni wa kiholela katika ufalme huo.
Syria: Mafunzo ya Silaha na Namna ya Kupigana Katika Mtandao wa Intaneti
Waasi nchini Syria wameanza kutumia YouTube ili kupeana mafunzo hasa kupitia 'Free Syrian Army Help' yaani 'Msaada wa Jeshi la Kuikomboa Syria'. Chaneli hiyo ina picha za video zipatazo 80 zikiliezea mbinu kama vile vita ya uso-kwa-uso, jinsi ya kutengeneza mabomu ya kutupwa kwa mkono, na jinsi ya kuwavizia maadui.
Morocco: Wanafunzi Wadai Marekebisho kwenye Mfumo wa Elimu
Mwezi Julai, kikundi cha wanafunzi wa nchini Morocco kilizindua ukurasa wa Facebook ulioitwa "Umoja wa Wanafunzi wa Morocco kwa ajili ya Mabadiliko ya Mfumo wa Elimu". Pungufu ya mwezi mmoja, kikundi hiki kilivuta uungwaji mkono mkubwa hasa kupitia mitandao ya kijamii.
Afrika ya Kusini: Yasherehekea Medali ya Kwanza ya Dhahadu Baada ya Miaka 8
Pongezi nyingi zimekuwa zikimimika kwa muogeleaji wa Afrika Kusini Cameron van der Burgh ambaye amechukua medali ya kwanza ya dhahabu baada ya nchi hiyo kupata matokeo mabaya katika mashindano ya Olimpiki ya mwaka 2008 yaliyofanyika jijini Beijing. Amekuwa mwanaume wa kwanza wa Afrika Kusini kushinda medali ya dhahabu katika mashindano ya uogeleaji ya Olympics.