Habari kutoka 30 Agosti 2012
Brazil: Mtoto wa Miaka 13 Aonyesha Matatizo ya Shule Kupitia Facebook
Diário de Classe [pt], ukurasa wa Facebook uliofunguliwa na Isadora Faber, aliye na miaka 13 na anayetokea Santa Catarina, Brazil, tayari umeonyesha kupendwa zaidi ya mara 176,000. Huku lengo lake likiwa ni “kuonyesha ukweli kuhusu shule za umma”, Isadora anaweka picha zinazoonyesha maeneo yanayohitaji kufanyiwa ukarabati katika shule yake pamoja na...
Kocha wa Timu ya Taifa ya Zambia Atunukiwa Ukaazi wa Kudumu
Zambia imewahi kuwa na makocha wengi wa kigeni wa timu ya Taifa ya soka, lakini ni Mfaransa Herve Renard, aliyeongoza timu hiyo hadi kushina Kombe la Washindi Barani Afrika mwaka 2012, aliyepata upendeleo wa pekee. Ili kutambua mafanikio yake haya, serikali imemtunuku ukaazi wa kudumu lakini uamuzi huo unaonekana kuwekewa chumvi ya kisiasa.
Tanzania/Malawi: Utafutaji Mafuta kwenye Ziwa Nyasa WachocheaMgogoro wa Umiliki
Taarifa kwamba Malawi inatafiti mafuta katika Ziwa Nyasa (linalojulilkana pia kama Ziwa Malawi) zimeibua mjadala motomoto. Wakati ambapo serikali ya Malawi inadai umiliki kamili wa ziwa hilo, Tanzania inataka mpaka utambuliwe kuwa katikati ya ziwa.