Habari kutoka Julai, 2012
Cameroon: Ndoto za Umeme kwa Ajili ya Maendeleo ifikapo 2035
Cameroon inatarajiwa kufikia hadhi ya soko linalokua kwa kasi ifikapo mwaka 2035 kupitia "mafanikio makubwa" ya hatua kwa hatua katika maendeleo ya miundombinu ya usafiri na nishati. Hata hivyo kufikiwa kwa malengo hayo ndani ya muda uliopangwa hakuonekani kuwashawishi wachambuzi wengi wa masuala ya kisiasa, kwa sababu tu changamoto zilziopo ni nyingi.
Angalia Moja kwa Moja Yanayojiri Sasa Hivi Katika Mkutano wa Global Voices
Mkutano wa Global Voices wa 2012 umeshafunguliwa muda mfupi uliopita katika jiji la Nairobi, nchini Kenya. Tungetamani sana kama ungeweza kujumuika nasi mkutanoni, lakini kama hilo haliwezekani, waweza pia ukatutazama moja kwa moja kupitia mtandao wa intaneti na pia tunaweza kujadiliana moja kwa moja.
Misri: Mubarak Afariki Dunia kwa Mara Nyingine
Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak amewahi kufa angalau mara moja kwa kila baada ya majuma machache tangu kuanza kwa mapinduzi ya Misri, yaliyouangusha utawala wake uliodumu kwa miaka 32. Watumiaji wa mtandao wanaitikia tetesi za hivi karibuni kuhusu afya yake.
Sudani: Maandamano Yachochea Kukamatwa kwa Mwanaharakati wa Twita
Maandamano makubwa yaliyofanyika nchini Sudani siku ya Ijumaa yalisababisha kukamatwa kwa wanaharakati wengi wa nchi hiyo, pamoja na watumiaji maarufu wa mtandao wa twita.
Cuba: Maandamano yafanyika Mara Mbili, Wengi Wakamatwa
Kikundi cha wanawake kijiitacho ‘wanawake wavaliao mavazi meupe’ (Ladies in White) kwa mara nyingine wametawala fikra za wanablogu wa Cuba waishio nje ya nchi. Maandamano ya amani ya kikundi hicho ambacho ni moja wapo ya vyombo vya upinzani vinavyoheshimika zaidi katika visiwa hivyo –pamoja na kukamatwa kwao mara kwa mara na vyombo vya dola –yanaendelea kuvuta hisia za watu. Mapambano ya hivi karibuni yalitokea mwishoni mwa juma lililopita wakati wanachama wa kikundi hicho walipojaribu kufanya maandamano mara mbili mjini Havana.
Tazama Picha za Afghanistan Ambazo Huwa Huzioni
Vyombo vingi vya habari vinavyovipoti hali inavyoendelea nchini Afghanistan hubeba taswira mbya. Kupitia miwani yao, Afghanistan huoneshwa kama nchi inayozama kwenye vimbi la mapigano na sura ya kijeshi. Wapiga kura kadhaa wanawasaidia watu kuona nchi hiyo iliyoathiriwa na vita lakini nzuri kwa mtazamo tofauti.