Nchini Misri, udhalilishaji wa kijinsia ni tatizo kubwa [1], na ndilo jambo linaloongozwa kupingwa na Wamisri. Maandamano yalifanywa na vijana wadogo wa Misri, wasichana kwa wavulana katika mji mdogo wa Nasr jijini Cairo mnamo tarehe 4 Julai kwa lengo la kutuma ujumbe kupinga udhalilishaji wa kijinsia.
Tangu mapinduzi yalipofanyika, Wamisri wanaotumia mtandao wa intaneti [2] na wasiotumia mtandao wa intaneti wamekuwa wakisimama imara kupinga udhalilishaji wa kijinsia pamoja na machafuko yatokanayo na kutokujali usawa wa binadamu. Mwezi Juni matembezi [3] ya kupinga udhalilishaji wa kijinsia yalishambuliwa [4]. Haikujalisha, harakati za kukabiliana na udhalilishaji huo zinaendelea.
Malengo ya maandamano ya Julai 4 yalilenga kuweka msimamo kuhusu kupinga udhalilishaji wa kijinsia na kudai usalama wa mitaa kwa wote. Maged Tawfiles [5] alikuwepo kwenye tukio na alipiga picha [6] zifuatazo (picha zote zimetumika kwa ruhusa):