Habari kutoka 16 Julai 2012
Hispania: Maandamano ya Wachimbaji Madini Yaungwa Mkono na Wananchi
Maelfu ya wananchi wa Uhispania wameungana na maandamano ya wachimbaji wa madini nchini humo, wakati waandamanaji hao walipowasili nchini Madrid baada ya kutembea kilometa 400 wakitokea kaskazini mwa nchi hiyo. Wachimbaji hao walishangazwa na kiwango cha hamasa kilichoonyeshwa, ambacho kiliongeza chachu ya kile ambacho sasa chaitwa 'usiku wa wachimbaji madini'