Habari kutoka 12 Juni 2012
Ethiopia: Ardhi, Historia na Haki katika Eneo la Gambella
Wanaharakati wa masuala ya ardhi wanatumia hati ya malalamiko ya mtandao, mtandao wa facebook na twita kufanya kampeni dhidi ya unyang’anyi wa ardhi nchini Ethiopia. Inaarifiwa kwamba wanakijiji kwenye jimbo msikini zaidi nchini humo, Gambella, wanalazimishwa kuhamia kwenye vijiji vilivyobuniwa na serikali ili kuwapisha wanaoitwa 'wawekezaji' wakubwa.
Misri: Maandamano ya Kukomesha Udhalilishaji wa Kijinsia Yavamiwa
Maandamano kudai kukomeshwa kwa udhalilishaji wa kijinsia yaligeuka kuwa shubiri baada ya wanawake waliokuwa wanahusika nayo kuvamiwa na kundi la wanaume wenye hasira kwenye viwanja vya Tahrir leo(June 8, 2012). Watu walioshuhudia tukio hilo walielezea maoni yao kupitia twita.
Kenya: Intani walipwe au wasilipwe?
Mada hapa ni kuhusu kama inafaaa au haifai kwa intani kulipwa,mjadala ulioanzishwa na @RobertAlai.
Brazili: Jarida Lawapa Nafasi Wasio na Makazi
Jarida la Ocas linalosambazwa katika mitaa ya mjini São Paulo pamoja na Rio de Janeiro tangu 2002, ni jarida ambalo husheheni habari ambazo hulitofautisha na vyombo vikuu vya habari nchini Brazil. Na linakwenda zaidi ya hapo. Aidha huwapa mwanzo mpya na fursa za kazi watu ambao hawana makazi na ambao wamo katika hatari ya kuangamia kijamii.