Habari kutoka 31 Mei 2012
Afrika: Kusherehekea Siku ya Ukombozi wa Afrika kwenye Mtandao wa Twita
Siku ya Ukombozi wa Afrika ni maadhimisho ya kila mwaka kukumbuka tarehe 25 Mei 1963 siku ambayo Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) ulianzishwa. Mwaka 2002 OAU ilianzisha mrithi wake aitwaye AU. Waafrika na marafiki wa Afrika wanasherehekea siku hiyo kupitia mtandao wa twita.
Zambia: Maoni na Hisia Tofauti baada ya Mwakilishi Kutolewa kwenye Mashindano ya Big Brother
Kuondolewa kwa mwakilishi wa Zambia, mwanamuziki anayefahamika zaidi kwa jina la Mampi, kutoka katika mashindano yanayoendelea ya Big Brother Africa, kumepokelewa kwa hisia na maoni tofauti miongoni mwa watumiaji wa mtandao. Big Brother Africa: StarGame ni toleo la saba la mfululizo wa mashindano hayo maarufu zaidi barani Afrika yanayoonyesha moja kwa moja kupitia televisheni maisha ya washiriki.