- Global Voices in Swahili - https://sw.globalvoices.org -

Tunisia: Miitikio Tofauti Kufuatia Kuingiliwa kwa Barua Pepe za Waziri Mkuu

Mada za Habari: Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, Tunisia, Harakati za Mtandaoni, Maandamano, Siasa, Uandishi wa Habari za Kiraia

Mnamo Aprili 8 “Anonymous Tunisia” kikundi kisichotambulisha majina ya wanachama wao nchini Tunisia (ambacho kinadai kuwa na uhusiano na kikundi cha watu “wasiojitambulisha” [1]) waingiliao mawasiliano ya watu kiliingilia mawasiliano [2] the ya barua pepe ya waziri mkuu wa Tunisia Hamadi Jebali [3]. Vuguvugu hilo lilipewa jina la utani la (“Achana na Tunisia yangu”) ambayo ni sehemu ya kampeni kuu iitwayo “Operesheni Rejeza Tunisia”.

[4]

Nembo ya Tunisia isiyojitambulisha

Katika mkesha wa mapinduzi mwaka 2011 wanachama wa kikundi hicho cha “wasiojitambulisha” waliotawanyika duniani kote walishambulia tovuti kadhaa za serikali katika kile kilichoitwa Operation Tunisia [5]. Mmoja wao hivi2,725 emails [6] wanachama wa chama tawala cha nchi hiyo cha Ennahda mtandaoni [7], ikiwa ni pamoja na mawasiliano ya waziri mkuu.

Namba za simu [8] zinazomilikiwa na maafisa nyeti wa serikali tangu wakati huo zimekuwa zikisambazwa katika kurasa za facebook. Serikali imekamatwa pabaya na mpaka sasa haijaweza kujibu chochote. Wakati huo huo, raia watumiao mtandao wamegawanyika kuhusu ufanisi wa hatua hiyo.

Bassem Meddeb katika hali ya kusisimuka, alituma ujumbe kupitia mtandao wa twita kuhusu kuperuzi maelfu ya barua pepe:

@bmeddeb [9]: Finalement #Anonymous nous a engagé comme détectives! #jbelileaks

Mwisho # Kikundi cha wasiojitambulisha kimetuajiri kama wachunguzi! #jbelileaks

Hmida Ben Jemmaa aliandika kwa kejeli:

@HBJtn [10]: Après le #JbeliLeaks, le bureau politique d'Ennahdha décide de correspondre avec des… pigeons voyageurs.

Baada ya #JbeliLeaks, kitengo cha siasa cha (chama cha) Ennahda kimeamua kuwasiliana kwa kupitia …njiwa waishio nyumbani
[11]

Nembo ya Operesheni Rejesha Tunisia

Hata hivyo, baadhi ya watumiaji wa twita walipingana na zoezi hilo la kuingilia mawasiliano ya watu.

Hmida Ben Jemmaa aliandika akipinga mashambulizi hayo, na kuongeza: [12]:

التدخّل الأجنبي في شؤوننا الدّاخلية خطّ أحمر
Kuingiliwa katika masuala yetu ya ndani ni kuvuka mipaka

Mwanafunzi wa Utabibu Amine Ghrabi alihoji mantiki ya Zoezi hilo linalofanywa na “watu wasiojitambulisha” na kutuma ujumbe:

@HendrixTN [13]: Petite pensée à tous ceux qui ont gâché leur matinée dominicale à fouiller la boite mail d'un incompétent confirmé ! #JbeliLeaks

Wazo dogo kwa wale wote waliharibu asubuhi zao za Jumapili hii kwa kuperuzi barua za watu ambao tuna hakika hawako timamu!

Alkimia alituma ujumbe huu:

@alkimia5550 [14]: بجدكم توا معملين تلقاو كارثة في #JbeliLeaks
Hivi kweli mnataka kutafuta janga katika kampeni ya #JbeliLeaks?

Na akaongeza:

@alkimia5550 [14]: Anonymous a menacé les Islamistes depuis qq mois.Il ne serait pas malin s'il n'a pas nettoyé

Kundi hili limekuwa likiwatishia Waislam wenye msimamo mkali kwa miezi michache iliyopita. [waziri mkuu] hangekuwa na werevu kama asingefuta barua zake zote kwenye anuani yake ya barua pepe

Mwanafunzi Imed Laaridh, anayeunga mkono chama tawala cha Ennahda, alituma ujumbe kwamba angegoma:

@ImedLaaridh [15]: On est peut être parti pour un tour de piratage réciproque. On trouvera de quoi passer le temps.. #TnPolitics #JbeliLeaks

Labda tumeanza awamu ya kwanza ya kuingiliana mawasiliano yetu. Ni jambo la kutufanya tupate cha kufanya…

Video ifatayo [Fr] iliwekwa na kikundi hicho. Mwanachama wa kundi hilo anazungumza kuhusu kuvuja kwa barua za waziri mkuu, na makarabrasha yanayotarajiwa zaidi muda mfupi ujao: