Habari kutoka 13 Aprili 2012
Tanzania: Mwigizaji Nyota wa Filamu, Steven Kanumba, Afariki Dunia
Tanzania ilimuaga mmoja wa wasanii wake maarufu na nyota wa tasnia ya filamu, Steven Kanumba, kwa maziko yaliyogubikwa na majonzi mazito mnamo tarehe 11 Aprili 2012. Alifariki alfajiri ya Jumamosi, akiwa na umri wa miaka 28, baada ya kile kilichodaiwa kuwa ugomvi wa kimapenzi na rafiki yake wa kike aitwaye Elizabeth Michael kwa jina maarufu “Lulu”.