Habari kutoka 8 Aprili 2012
Taiwan: Kufukuzwa kwenye nyumba kwa nguvu kwa familia kwaitia dosari Sheria ya Ufufuaji Miji
Kufukuzwa kwa kinyama kwa familia ya Wang kulikotekelezwa na serikali ya Jiji la Taipei kulionyesha jinsi haki za raia zilivyo dhaifu mbele ya miradi ya ufufuaji mji. Kumekuwepo na maoni mengi yanayotaka Sheria ya Ufufuaji Miji irekebishwe.
Congo (DRC): Video zasaidia kumtia hatiani Thomas Lubanga kwa uhalifu wa kivita
Mnamo tarehe 14, Machi, mahakama ya kimataifa ya makosa ya kivita ilimtia hatiani Thomas Lubanga, kiongozi wa zamani wa waasi Kongo (DRC) Mashariki, kwa kosa la kuwatumia watoto katika vita. Jaji alisema picha za video zilizoonyesha mahojiano na askari hao watoto ziliziongeza uzito wa ushahidi ulioisaidia mahakama kutoa hukumu.