Viti kadhaa vilivyo wazi katika vyuo vikuu vya Iran vilikaliwa rasmi na wanafunzi ambao hivi sasa wametoweka. Wengine wananyimwa elimu kutokana na sababu za kidini, kama vile waumini wa Baha'i [1] dini yenye waumini wachache [2], wengine wamefungwa jela kwa sababu za kisiasa, wengine wameuawa mitaani, au wamelazimishwa kuondoka Iran. Katika mazingira ya kawaida, kuna wanafunzi ambao wamefukuzwa tu.
Mwaka huu Tahkim Vahdat [3], kikundi cha upinzani cha wanafunzi kinachoongoza, kiliitisha kampeni ya “viti visivyokaliwa” duniani kote, mnamo desemba 7,siku ya wanafunzi wa Iran [4],ili kukumbuka wale wote waliokosa tumaini la kupata elimu. Ukurasa wa Facebook [5] ulianzishwa, na filamu nyingi zilipandishwa kwenye YouTube, ili kuonyesha mshikamano kwa wanafunzi waliopoteza na wanaokandamizwa nchini Iran. Hizi ni tatu kati hizo filamu.
Chuo kikuu George Washington, USA
Barcelona, Hispania
http://www.youtube.com/watch?feature=player_embedded&v=4535gGdL-qQ [6]
Ujumbe kutoka Kanada kwa mwanafunzi aliyefungwa jela