Makala hii ni sehemu ya habari maalumu za Tetemeko la Japani 2011 [1].
Kufuatia tetemeko kubwa kuwahi kutokea nchini [2], Japani imekumbwa na tsumani mbaya zaidi iliyowahi kutokea. Watu wengi nchini kote wameganda kwenye luninga zao wakati vipande vya habari vinavyoonesha tsunami lenye urefu wa zaidi ya mita 7 kwenda juu likisomba magari na majengo. Wakati huo huo, maeneo mengine ya dunia yanajiandaa kwa matukio mabaya zaidi, Hawaii imetoa amri ya kuhama kutoka kwenye maeneo ya pwani [3] na tahadhari zimetolewa katika nchi zisizopungua 20 [4]. Jarida la The Guardian linatoa habari za mpya kadiri zinavyojitokeza [5] kuhusiana na janga hilo.
http://www.youtube.com/watch?v=rWgvX1FGK4I [6]
http://www.youtube.com/watch?v=lSimeWFiuYc [7]
Picha ya wimbi kubwa la bahari mjini Ibaraki [8] (kupitia @gakuranman [9]):
Baadhi ya ujumbe kwenye twita.
Tinystar323 anaandika [10]:
津波は「波」じゃなくて、「コンクリートの壁が猛スピードで突っ込んでくる物」だと思って下さい。人間にどうにか出来る代物じゃないです。絶対に興味本位で見に行ったりしないで下さい。
Taarifa isiyothibitishwa kutoka @nishi_0024 [11] ikidai kwamba kituo cha mkutano cha Pacifico Yokohama hakipokei tena watu:
【緊急拡散】パシフィコ横浜は津波の危険があるため、受け入れ中止だそうです!
Kutoka @edamamicky [12], mwathirika wa tsunami:
津波被害あり。自宅2階にて母と弟と近所の男性一名と救助を待っています。怪我はありません。1階は浸水して自力では外に出れません。電話も繋がりません。
Kwa habari za hadi dakika iliyopita kuhusiana na hali ya mambo baada ya tetemeko, fuatilia chanzo rasmi cha habari [13] cha NHK.
Makala hii ni sehemu ya habari maalumu za Tetemeko la Japani 2011 [1].