Julai, 2010

Habari kutoka Julai, 2010

Uganda: Wanablogu Washtushwa na Milipuko ya Mabomu

Mashabiki wa soka kote ulimwenguni walikusanyika kwenye kumbi za baa na migahawa ili kushuhudia mechi ya fainali za Kombe la Dunia usiku wa Jumapili iliyopita. Nchini uganda usherehekeaji huu ulikatishwa pale milipuko ya mabomu iliposambaratisha maeneo mawili maarufu kwa sherehe za mpaka majogoo jijini Kampala, mji mkuu wa nchi hiyo.

15 Julai 2010

Naijeria: Nani Amemfanya Rais Abadili Msimamo — Facebook au FIFA?

Baada ya kupokea mamia ya maoni kwenye ukurasa wake wa Facebook page, Rais wa Naijeria alibadili uamuzi wake tata wa kuifungia timu ya taifa ya nchi hiyo. Lakini je ni kweli kwamba kubadilika huku kwa moyo wa Jonathan kulitokana na maoni ya raia waliopaaza sauti zao zenye hasira katika Facebook? Au ulitokana na msukumo wa shirikisho lenye nguvu la mpira wa miguu?

13 Julai 2010

Angola: Hapo Zamani za Kale Katika Roque Santeiro

Maendeleo yanayoukumba mji wa Luanda unaliwajibisha moja ya eneo la biashara linalotembelewa zaidi mjini humo, eneo ambalo hutengeneza maelfu ya dola kwa siku. Soko la Roque Santeiro limo mbioni kufunga "milango" yake na kufunguliwa katika eneo la kisasa na lenye hadhi, huko Sambizanga.

3 Julai 2010