Habari kutoka 27 Februari 2010
Lebanon: wanablogu washinikiza jarida la Daily Star kubadilika
Wanablogu wa Lebanon wanapiga kampeni ya kwenye mtandao ili kulishinikiza gazeti pekee la kwenye wavuti kurekebisha tovuti yake. Mwanablogu mmoja amefanya jitihada kubuni tovuti ya kuiga - ambayo wenzake wanatumaini itahimiza mabadiliko katika gazeti la Daily Star, na kuibadili 'boti moshi ya Kirusi ya miaka ya 1920' kuwa meli ya karne ya 21 ya abiria.
Kadri Liberia inavyotulia, vijana waanza kuzungumzia ngono
Kadri Liberia inavyoendelea kutoka kwenye vita ya kutisha ya wenyewe kwa wenyewe, wengi wanahofu mchanganyiko wa umaskini uliokithiri na maamuzi yenye hatari ya ngono vitaongeza kiwango cha VVU/UKIMWI na idadi ya mimba zisizotarajiwa.
Ethiopia: Wanablogu walitetea Shirika la Ndege la Ethiopia baada ya ajali ya ndege
Wanablogu waishio Ethiopia wameharakia kuitetea rekodi ya usalama wa safari za ndege za nchi hiyo siku ya Jumatatu baada ya ndege moja kuanguka karibu na Beirut, ikihofiwa kupoteza maisha ya watu wote 90 waliokuwepo.
Ghana: Mkuu wa Mkoa, Kofi Opoku-Manu, Anapoteza Umaarufu?
Mkuu wa Mkoa wa Ashanti, Kofi Opoku-Manu, hivi karibuni alionja joto ya jiwe kutokana na matamshi aliyoyatoa kwenye hotuba yake kwa mashabiki wa chama tawala, Nationa Democratic Congress (NDC) tarehe 6 Januari. Kwa mujibu wa Ato-Kwemena Dadzie, Opoku-Manu “aliwasihi mashabiki wa chama kutumia ghasia kusuluhisha tofauti zao.”