17 Februari 2010

Habari kutoka 17 Februari 2010

Ghana: Mapendekezo ya Kuvutia Kwenye Mapitio ya Katiba

Mwaka 2008, wakati wa Uchaguzi wa rais, wagombea waliwaahidi Waghana kuwa wangeitazama tena katiba ya nchi hiyo. Jambo lililoifanya ahadi hii kuonekana kama ni ya kweli lilikuwa ni nia ya wagombea – pamoja na Rais John Atta Mills – ya kuwashirikisha Waghana katika mchakato huo wa kuitathmini katiba. Inaonekana kuwa rais ametimiza ahadi hiyo, na sasa mapendekezo mapya yanachochea mijadala ya kuvutia.

India: Ugaidi Waikumba Pune

  17 Februari 2010

Mnamo majira ya saa 1:30 jioni (Februari 13, 2010) mlipuko wa bomuuliua watu 9 na kuwajeruhi wengine 57 katika mgahawa maarufu kwa watalii uliopo katika mji wa Magharibi wa Pune, India. Hisia ziko juu huku wanablogu na watumiaji wa twita wakitoa maoni.