Habari kutoka 26 Januari 2010
Haiti: Kituo Cha Habari Chazinduliwa Kwa Ajili Ya Uanahabari wa Haiti
Réseau Citadelle anatangaza kuzinduliwa kwa Kituo Cha Habari, mradi unaotoka kwa Wanahabari Wasio Na Mipaka pamoja na Quebecor, wenye lengo la kuwezesha kazi za wanahabari wa ndani na wa nje ambao wako nchini Haiti, na pia kuunda ubia kati ya Asasi Zisizo za Kiserikali na Vyombo vya Habari.
Lebanoni: Watu 90 Wanahofiwa Kufariki Baada ya Ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia Kuanguka Baharini
Rambirambi zilimiminika kwenye Twita baada ya ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia kuanguka kwenye (bahari ya) Mediterani dakika chache baaday ya kupaa ikitokea Beirut, Lebanoni. Watu wote 90 waliokuwemo wanahofiwa kuwa wamekufa baada ya ndege hiyo kushika moto katika kimbunga cha radi na kuangukia baharini.
China: Tangazo la Google Kusahihisha Uvumi Limezua Utabiri Mwingine
Tangazo la hivi karibuni la Google.cn linasema kuwa uvumi kuhusu kujitoa kwake ni uvumi tu. Hata hivyo, utabiri zaidi ulijitokeza, ukiuliza iwapo uamuzi wa Google unalenga kuficha kushindwa kwake kibiashara, au unalenga kutumikia maslahi ya kisiasa.