Habari kutoka 9 Januari 2010
Picha ya Dunia Katika Siku ya Kupinga Rushwa Duniani
Katika matayarisho ya uzinduzi wa mtandao wa teknolojia na Uwazi, hii ni makala ya kwanza kabisa katika mfululizo wa makala ambazo zitavinjari mada zinazohusiana kwa kupitia macho ya wanablogu wa dunia.
Georgia: Hebu Tuongelee Tendo la Ngono…
Pengine mada iliyotawala katika vyombo vya uanahabari wa kijamii vya Georgia haikuwa siasa, uchaguzi, matatizo, matetemeko ya ardhi au majanga. Badala yake, mada iliyojadiliwa sana ilikuwa inahusu kipindi kipya cha televisheni, Ghame Shorenastan. Kinachoonyeshwa kwenye Imedi TV, jina la kipindi hicho linatafsirika kama Usiku pamoja na Shorena na kinaongelea mada zinazohusu tendo la ngono.
Msumbiji: Kifo Cha Mradi Mkubwa wa Mazao Nishati
Mwishoni mwa mwezi Disemba, Baraza la Mawaziri la Msumbiji lilitoa tamko muhimu. Kibali cha kutumia Hekta 30,000 za ardhi kwa kampuni ya mazao nishati (biofuels) Procana, kimebatilishwa. Shauri la Mradi wa Procana, ulipo kwenye eneo kubwa linalopakana na Mbuga ya Taifa ya Limpopo ambayo imetanda mpaka nje mpaka wa nchi, lilikuwa na utata pamoja na mvutano mkubwa tangu (shauri hilo) lilipoanza mwanzoni mwa mwaka 2007.
Australia: Mauaji ya Mhindi Yazua Mzozo
Mauaji ya mtu mwenye asili ya India mjini Melbourne yamewasha tena mjadala kuhusu ubaguzi wa rangi nchini Australia na usalama wa wanafunzi kutoka ng’ambo. Kadhalika yameathiri uhusiano kati ya Australia na India. Mwandishi wa GV Kevin Rennie anakusanya maoni ya wanablogu wa Australia.