Disemba, 2009

Habari kutoka Disemba, 2009

Morocco: Kusherehekea Idi katika Sehemu za Mashambani

Wikiendi hii iliyopita, Wamoroko walisherehekea Eid Al-Adha. Wanablogu walioko sehemu za vijijini nchini Moroko wanasimulia simulizi zao kuhusu Eid ya mwaka huu. Kwa kuwa upatikanaji wa intaneti upo sehemu chache n amara nyingi ni wa aghali mno nje miji mikubwa, wengi wanaoblugu kutokea sehemu za mashamba ni Wafanyakazi wa Amani wa Kujitolea (PCVs) na kwa hiyo wako katika nafasi ya kuweza kutoa mitazamo kama wageni kutoka nje… walioko ndani.

Indonesia: Sarafu za Kudai Haki

  8 Disemba 2009

Raia wa mtandaoni (Netizens) wamezindua kampeni ya kukusanya fedha zilizo katika muundo wa sarafu ili kumuunga mkono Prita Mulyasari, mama wa nyumbani raia wa Indonesia aliyeandika malalamiko yake mtandaoni dhidi ya hospitali iliyotoa huduma mbaya, na ambaye alipatikana na hatia na mahakama moja ya kosa la "kuchafua jina" la hospitali hiyo binafsi.

Guinea: Jaribio la Kumuua Kiongozi wa Kijeshi Dadis Camara

Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari, Kapteni Dadis Camara, kiongozi wa kikundi cha jeshi kilitwaa madaraka nchini Guinea mwezi Disemba 2008, alipigwa risasi na kujeruhiwa na mmoja wa wasaidizi wake jana mjini Conakry. Wasomaji wengi wa RFI wanaodai kuwa Camara anawajibika kwa mauaji ya waandamanaji wa upinzani yaliyotokea tarehe 28 Septemba, wanaoana kuwa haki imetendeka.

Guatemala: Kuvunja Milango ya Madanguro

  6 Disemba 2009

Blogu inayojulikana kama Noticias para Dios inatoa habari za ndani, kama vile mambo yenyewe yanavyotokea pasipo kuficha kitu, kuhusu maisha ya kila siku ya mwanasheria wa Ki-Guatemala anayejaribu kuwaokoa watoto kutoka kwenye madanguro ambako wamekuwa wakiishi baada ya kuchukuliwa kutoka makwao.

Mchakato wa Amani Nepal Unayumba

  6 Disemba 2009

Mchakato nyeti wa kuleta amani nchini Nepal unasitasita katikati ya mapambano yanayozidi kuongezeka kati ya watu wa kundi la ki-Mao na serikali. Kundi la ki_Mao linatishia kuitisha mgomo usio na kikomo kama madai yao hayatatekelezwa.